Header AD

SHUGHULI ZA KUTAMBULIWA MAITI ZILIZOOKOLEWA KATIKA AJALI YA MELI ZIKIENDELEA ZANZIBAR

Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli ya Skagit iliozama hapo jana zikitambuliwa na Ndugu zao na kuruhusiwa Kuzichukuwa kwa ajili ya Kufanya taratibu za mazishi hapo katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.
Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Learnhat Alfonso wakatikati akionekana na huzuni Baada ya kuziona Maiti zilizookolewa katika Meli iliozama hapo jana katika Bahari ya Chumbe Zanzibar.Balozi alifika katika Viwanja vya Maisara ili kuona namna shughuli za kushughulikia maiti zinavyoendelea.
Mama alietambulika kwa Jina la Bitatu Uyelo ambae amenusurika na Kupoteza Mtoto wake wa miezi tisa katika Ajali ya Meli ya Skagit iliozama hapo jana katika Bahari ya Chumbe ikitokea Dare es salaam.
Waziri wa Mamboya ndani wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Emanuel Nchimbi alifikakatika Eneo lililohifadhiwa Maiti wa Ajali ya Meli ya Skagit ili kutambuliwa na Ndugu zao na Kupata maelezo kwa Daktari Kiongozi hayupo pichani Hapo katika Viwanja Vya Maisara Zanzibar.Picha Kwa Hisani Ya Michuzi Blog
Reviewed by crispaseve on 07:42 Rating: 5

No comments

Post AD