Header AD

WASANII SUPER J. NA NEYLEE WAIBUKA WASHINDI WA SERENGETI FIESTA SUPER NYOTA MKOA WA MBEYA

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 "Bhaasi" Bwana Sebastian Maganga akiwapongeza washindi wa Serengeti  Fiesta Super Nyota Super J. kulia na Neylee, mara baada ya wasanii hao  kuibuka washindi katika shindano hilo lililofanyika usiku huu kwenye klabu ya Vibes jijini Mbeya, wasanii hawa watauwakilisha mkoa wa Mbeya katika matamasha mbalimbali ya Serengeti Fiesta mikoani
Mtangazaji wa Clouds Antu Mandoza akizungumza jambo mara baada ya kuwakabidhi zawadi zao za kreti mbili za bia aina ya Serengeti Lager kutokana na ushindi wao katika shindano hilo lililomalizika usiku hu jijini Mbeya.
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 Bw. Sebasttian Maganga akitangaza washindi katika shindano la Serengeti Fiesta Super Nyota lililomalizika usiku huu kwenye klabu ya Vibes jijini Mbeya.
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza kwenye klabu ya Vibes ili kushuhudia shindano hilo wakifuatilia kwa makini wakati wasanii hao walipokuwa wakishindana.
Msanii Super J. akifanya vitu vyake mbele ya mashabiki waliojitokeza katika klabu ya Vibes usiku huu.
Msanii 1 Rich akionyesha uwezo wake jukwaani wakati wasanii wa muziki wa kizazi kipya Bongofleva waliposhindana kuimba katika shindano la Serengeti Fiesta Super Nyota lililomalizika usiku huu kwenye klabu ya Vibes jijini Mbeya
Mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wakiwashangilia wasanii walipokuwa wakishindana katika shindano la Serengeti Fiesta Super Nyota.
Kutoka kulia wa pili ni Shafii Daudam Sebastian Maganga na Antu Mandoza wakifurahia jambo pamoja na mshabiki wengine waliohudhuria katika shindano hilo.
Mashabiki wapata burudani ya muziki kabla ya kuanza kwa shindano hilo.
You might also like:
Reviewed by crispaseve on 11:55 Rating: 5

No comments

Post AD