Header AD

WAZIRI WA HABARI, DKT. FENELLA AMTEUA DKT. SEWANGI KUWA KATIBU MTENDAJI BAKITA


Dkt. Fenella Mukangara, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

NA MAGRETH KINABO- MAELEZO

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara, amemteua Dkt. Selemani Sewangi (55) kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa  (BAKITA).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Waziri wa wizara  hiyo, uteuzi huo umeaanza rasmi  Julai Mosi mwaka huu.

Taarifa hiyo ilifafanua kuwa Dkt. Sewangi  ni Mhadhiri Mwandamizi wa Taasisi za Kiswahili (TATAKI) kutoka  Chuo Kikuu cha Dares Salaam.

Dkt. Sewangi anachukua nafasi hiyo iliyoachwa na Dkt. Anna Kishe, aliyestaafu kwa mujibu wa sheria.
Reviewed by crispaseve on 11:31 Rating: 5

No comments

Post AD