YANGA WATUMIA VYEMA MAKOSA YA AZAM NA KUICHAPA MAGOLI 2-0 NA KUIBUKA MSHINDI WA KAGAME CUP
Kipre Cheche kulia Mchezaji wa timu ya Azam FC akikokota mpira mbelea ya beki wa Yanga Nidir Haroub Canavaro wakati wa mchezo wa fainali ya kombe la Kagame inayofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii, mpira umekwisha na timu ya Yanga imefanikiwa kutetea kombe la Kagame kwa mara ya pili mfurulizo baada ya kuitandika timu ya Azam FC goli 2-0 jioni hii.
Mshambuliaji wa Timu ya Yanga, Hamis Kiiza akishangila goli la kwanza la timu yake wakati wa Fainali za Ligi ya Kagame iliyochezwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Kiiza akishangilia bao la kwanza alilofunga dakika ya 44
Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao la kuongoza
Said Bahanuz wa Yanga akimtoka Beki wa Azam,Aggrey Moris.
Mshambuliaji wa Yanga,Hamis Kiiza akiondoka na mpira huku mlinzi wa Azam,Jabir Aziz akimkimbiza kwa kutaka kumzuia mshambuliaji huyo.
Mlinzi wa timu ya Azam,Said Moradi akiwania mpira na Mshambuliaji wa Timu ya Yanga,Said Bahanuz wakati wa mchezo wa fainali ya Mashindano ya Cecafa Kagame cup.
Mashabiki nao hawakua nyuma wakati wa ushangiliaji
Kabla ya Mechi kuanza
Kipa wa Azam akiokoa hatari langoni mwake.
Reviewed by crispaseve
on
03:05
Rating:
Post a Comment