MWANAMUZIKI WA NIGERIA RAPPER WIZ KID ANUSURIKA KUFA BAADA YA GARI ALILOKUWA ANAENDESHA KUPATA PANCHA NA KUPINDUKA.
Pichani ni gari aina ya Porsche Panamera analomiliki Rapper Wiz kid muda mfupi baada ya kupata ajali.
Rapper mdogo ambaye amejipatia umaarufu
mkubwa anayefahamika kwa jina la Wiz Kid siku ya tarehe 15 mwezi huu
jumamosi asubuhi alinusurika kufa baada ya gari alilokuwa anaendesha
aina ya Porsche Panamera kupata pancha na kufanya gari hiyo kukosa
muelekeo na kuanguka.
Chanzo kinasema rapper huyo alikuwa
ametoka kwenye party katika hoteli ya Oriental , Lekki, jijini Lagos
ambapo kwenye gari hiyo kulikuwa na marafiki zake wachache, pia rapper
huyo amepata nafasi ya kumshukuru Mungu kwa kumuepusha na ajali hiyo
katika mtandao wa kijamii wa twitter.
Source: .dstv.com
Reviewed by crispaseve
on
13:02
Rating:
Post a Comment