HIVI NDIVYO DAVID MOYES ALIVYOFUNGASHIWA VIRAGO, GIGGS KUKAIMU NAFASI YAKE KWA MUDA
Bodi ya Manchester United imethibitisha rasmi kusitisha
mkataba wake na kocha David Moyes aliyekuwa akikinoa kikosi hicho cha
mashetani wekundu, huku kipigo cha juzi kutoka kwa Everton katika dimba
la Goodson park cha mabao mawili kikitajwa kuwa mojawapo ya sababu
kubwa zilizochangia kupigwa chini kwa kocha huyo na kufanya kufifia kwa
ndoto za vijana hao wa Glazer kucheza klabu bingwa barani ulaya hapo mwakani.
Huku kampuni kama vile ya NIKE inayowafadhili vifaa vya
michezo ikionekana kama kutaka kukimbia kutokana na kutoridhishwa na
mwenendo mzima wa timu kwa hivi sasa.
Nafasi ya Moyes imetajwa kukaimiwa na mchezaji nguli wa timu iyo, Ryan Giggs mpaka pale atakapopatikana kocha mpya.
Awali Moyes alichaguliwa kuchukua nafasi ya umeneja na kocha
wa zamani wa United, Sir Alex Ferguson ambaye alikuwa ameshikilia hiyo
nafasi kwa takribani muda wa miongo miwili na nusu, huku akiamini kuwa
ndiye kocha ambaye angeweza kuleta mabadiliko katika timu hiyo sambamba
na kuwa na historia ya kuka na timu kwa muda mrefu.
David Moyes alipewa mkataba wa miaka sita wa kuinoa
Manchester United akiwa tayari ameshaongoza jumla ya michezo 51 tangu
ajiunge na kikosi hicho cha Old Trafford.
Katika mechi 51 ambazo tayari amezisimamia, ameweza kushinda
mechi 27, amekwenda sare mechi 9 na kufungwa mechi 15 na hivyo kufanya
asilimia ya ushindi kuwa 52.94, hali inayoonyesha matokeo mabaya katika
historia ya Manchester.
Mpaka sasa bado hakujakuwepo na taarifa za hatima ya kocha
huyo kama ataendelea kulipwa mshahara wake ndani ya kipindi cha miaka
sita iliyobakia kama jinsi inavyokuwa kwa makocha wengine pindi wanapokuwa wamefukuwa kwenye vilabu walivyokuwa wakifundisha.
HIVI NDIVYO DAVID MOYES ALIVYOFUNGASHIWA VIRAGO, GIGGS KUKAIMU NAFASI YAKE KWA MUDA
Reviewed by crispaseve
on
00:24
Rating:
Post a Comment