TETESI ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA PSQUARE, PETER NA PAUL WADAIWA KURUSHIANA MAKONDE, KISA???
Ule
msemo usemao Adui anaweza kuwa rafiki na rafiki akawa adui
umejidhihirisha wazi wazi kupitia familia ya muziki kutoka nchini
Nigeria ‘Psquare’ inayoundwa na mapacha wawili waliozaliwa tumbo moja,
Peter na Paul Okoye kudaiwa kuingia katika mgogoro uliopelekea kuzichapa
kavukavu walipokuwa kwenye mazoezi jumatano iliyopita hali
iliyopelekea wacheza shoo wao kuamulia na kufanikiwa kuwatenganisha.
Kwa mujibu wa taarifa zinadai kwamba, kumekuwa na mvutano wa
familia ya Okoye huku mke wa Peter aitwae Lola Omotayo akitajwa kuwa
ndio chanzo cha mapacha hao kuingia kwenye ugomvi hali iliyopelekea
kuzuka kwa tetesi kuwa huenda ukawa ndio mwanzo wa kusambaratika kwa
kundi hilo lililodumu na kupata mafanikio makubwa kimataifa kupitia
sanaa ya muziki kwa kipindi cha takribani miaka 10.
Chanzo kiliendelea kufunguka kuwa meneja wa kundi hilo, Jude
Okoye’ ambaye ni kaka mkubwa wa Psquare na mke wa Peter kudaiwa
kutopikia chungu kimoja, hali iliyompelekea kutohudhuria sherehe yao ya
kimila iliyofungwa mwaka jana jijini Lagos, Nigeria.
Peter na Paul waliopanga kufanya sherehe jijini Dubai,
walijikuta wakifikia hatua ya kubishana huku upande mmoja ukitaka kaka
yao ahudhurie harusi hiyo licha ya kuwepo kwa vijimaneno kutoka kwa mke
wa Peter ‘Lala’ kutotaka Jude kuhudhuria sherehe yao.
”After over 10yrs of hard work, it’s over. Am done”. ilikuwa ni moja ya ujumbe alioandika Jude Okoye kupitia ukurasa wake wa Twitter.
TETESI ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA PSQUARE, PETER NA PAUL WADAIWA KURUSHIANA MAKONDE, KISA???
Reviewed by crispaseve
on
03:03
Rating:
Post a Comment