Header AD

WAZIRI MKUU APIGIA KURA VIVUTIO VYA TANZANIA

 Waziri Mkuu Mh. Mizengo Peter akipata maelekezo ya namna ya kupiga kura yake kutoka kwa Meneja wa Tawi la Bodi ya Utalii Tanzania(TTB) Arusha Bw. Wily Lyimo muda mfupi kabla ya kupiga kura yake katika kituo cha Mikutano cha AICC mjini Arusha hivi karibuni.
……………………………………..

Na: Geofrey Tengeneza

 Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda  hivi karibuni amepiga kura yake ya kuvichagua vivutio vitatu vya Tanzana katika shindano linaloendelea hivi sasa la kutafuta maajabu Saba ya asili ya Afrika.

 Waziri Mkuu alipiga kura yake wakati wa mkutano wa tano wa wadau wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa mikutano wa AICC mjini Arusha ambapo Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) iliweka kituo cha kupigia kura kwa njia ya mtandao wa komputa (internet). Waziri Mkuu alivipigia kura vivutio hivyo vitatu ambavyo ni Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Kreta ya Ngorongoro ili viweze kuwa miongoni mwa maajabu Saba ya Asili barani Afrika. Viongozi wengine waliopiga kura zao wakati wa mkutano huo katika kituo hicho cha Bodi ya utalii Tanzania ni pamoja na Waziri wa Kazi na Ajira  Mh.Gaudensia Kabaka, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mh.Henry Mwanri na viongozi mbalimbali wa LAPF.

 Bodi ya Utalii Tanzania hivi sasa inaendesha kampeni kamambe ya kuwahamasisha watanzania kuvipigia kura vivutio hivyo, na katika mkutano huo iliamua kupiga kambi katika kituo hicho cha mikutano ya Kimataifa cha AICC kwa lengo la kuwahamashishawajumbe wa mkutano huo na kuhakikisha wale ambao hawajapiga kura wanapiga kura zao katika kituo hicho hapo AICC zoezi ambalo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Tanzania ni nchi pekee barani Afrika iliyoingiza vivutio vingi katika shindano hilo ambapo imefanikiwa kuiongiza vivutio vitatu.
Reviewed by crispaseve on 04:09 Rating: 5

No comments

Post AD