JIJI LA TEXAS NCHINI MAREKANI LAKUMBWA NA MLIPUKO, WATU ZAIDI YA 100 WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA

Mlipuko umetokea katika kiwanda
cha kutengeza mbolea karibu na Waco, katika jimbo la Texas nchini
Marekani huku idadi kubwa ya watu wakijeruhiwa na wengine kukwama ndani
ya kiwanda hicho

Moshi mkubwa uliokena ukipanda
juu kutoka katika eneo la mlipuko. Wazima moto na magari ya Ambulance
pamoja na helikopta sita zilionekana zikiwasaidia majeruhi.

Wazaima moto hapa wakipambana na
moto huo karibu na kiwanda hicho. Majengo kadhaa yaliharibiwa vibaya
mengina yakiwa katika maeneo jirani.

Wazee waliokuwa katika makao
jirani ya kuwatunza wazee, walihamishwa mara moja. Kulikuwa na ripoti
kuwa wazima moto walikuwa wanajaribu kuzima moto wakati mlipuko huo
ulipotokea.

Uharibifu mkubwa ulitokea kwa
makao ya kuwahifadhi wazee. Mlipuko ulitokea nyakati za usiku wa kuamkia
leo
Zaidi ya watu 100 wamejeruhiwa katika mulipuko
uliotokea kwenye kiwanda cha mbolea kilichoko Kaskazini Magharibi mwa
eneo la Waco, jimbo la Texas. Wengi wamekwama ndani ya majengo
yanayendelea kuteketea kufuatia mulipuko huo.
Meya wa Mji kulitokea mulipuko huo, Tummy Muska
ameelezea kutokea moto mkubwa uliolipuka sawa na bomu. Mulipuko huo
umeharibu majengo ya kiwanda hicho, makaazi ya karibu kikiwemo kituo
kimoja cha afya.
Wazima moto, magari ya kubebea wagonjwa na helikopta sita zimetolewa kushughulikia majeruhi na kutuliza hali ya sasa.
Majengo kadhaa yameendelea kuteketea karibu na
kiwanda hicho cha mbolea.Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema
zinasea kuna watu waliopoteza maisha.
Dean Wilson wa idara ya usalama ya Texas amesema nyumba 75 karibu na jengo hilo ziliharibiwa kabisa.
Amesema kufikia sasa hawezi kuthibitisha vifo
vyovyote. Watu 38 wameripotiwa kua katika hali mahututi. Makundi ya
wokozi yameanza kufika nyumba hadi nyingine kuwaokoa majeruhi na kutoa
huduma ya kwanza.
Kituo cha Dharura kimewekwa kwenye uwanja wa
mpira ulioko karibu.Gavana wa Texas amesema afisi yake imetoa raslimali
zake kusaidia katika juhudi za wokozi.
Chanzo: BBC SWAHILI
WATANZANIA WASHINDWA KUFANYA VIZURI KIPINDI CHA TANO CHA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE
Washindi
wa kipindi cha tano cha Guinness Football Challenge Ken Muturi
(kushuto) na Chris Mwamgi(kulia) wakishangilia ushindi walioupata huku
wakiwa wamebeba pesa taslimu walizojishindia katika shindano hilo jana
usiku na pembeni ni mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho Lary
Asengo(anayepiga makofi kulia).
………………………………………………..
Jana
usiku kupitia Televisheni za ITV na Clouds TV timu ya Tanzania
ilishindwa kutumia nafasi ya kipindi cha mwisho cha mashindano ya “Guinness
Football Challenge” katika hatua ya Afrika Mashariki baada ya kutolewa
na timu kutoka Kenya. Rangi nyekundu imeonekana kuwa ni rangi ya bahati
kwa timu za Kenya kwani hii ni timu ya nne kutoka Kenya kufanikiwa
kufuzu kuingia hatua ya Pan-African GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGETM.
Kenneth Mukuri na Chris Mwamgi ndio walioibuka washindi jana usiku
kwani walifanikiwa kufika katika hatua ya mwisho ya kulenga ukuta wa
pesa wa Guinness ambapo walijishindia dola za kimarekani 1,500.
Ni
vipi Kenneth na Chris wataweza kumudu hatua ya Pan-African? Sasa wana
nafasi ya kuiwakilisha nchi yao katika mashindano ya Pan-African ambapo
watakutana na wawakilishi pekee kutoka Tanzania, Daniel Msekwa na
Mwalimu, washiriki kutoka Uganda Alex Muyobo na Ibrahim Kawoova pamoja
na wenzao kutoka Kenya,Francis Ngigi na Kepha Kimani(washindi wa kipindi
cha 2), Kenneth Kamau na Wills Ogutu(washindi kipindi cha 3) na
Ephantus Nyambura na Samuel Papa(washindi kipindi cha 4).
Timu
hizi tano zitakua uwanjani kutimiza malengo yao, ambapo watakutana uso
kwa uso na washiriki kutoka Ghana na Cameroun kuonesha ni nani ana
maarifa zaidi na ujuzi wa kusakata kabumbu, hata kuvishwa ubingwa wa
Pan-African na kuondoka na dola za kimarekani 250,000.
Usikose kuangalia mashindano haya kupitia televisheni za ITV na Clouds TV huku ukiburudika na kinywaji cha GUINNESS.
Tafadhali kunywa kistaarabu – Hairuhusiwi kwa wenye umri chini ya miaka 18.

Post a Comment