Header AD

JIJI LA TEXAS NCHINI MAREKANI LAKUMBWA NA MLIPUKO, WATU ZAIDI YA 100 WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA

 
Mlipuko umetokea katika kiwanda cha kutengeza mbolea karibu na Waco, katika jimbo la Texas nchini Marekani huku idadi kubwa ya watu wakijeruhiwa na wengine kukwama ndani ya kiwanda hicho 
 
Moshi mkubwa uliokena ukipanda juu kutoka katika eneo la mlipuko. Wazima moto na magari ya Ambulance pamoja na helikopta sita zilionekana zikiwasaidia majeruhi.
Wazaima moto hapa wakipambana na moto huo karibu na kiwanda hicho. Majengo kadhaa yaliharibiwa vibaya mengina yakiwa katika maeneo jirani.
Wazee waliokuwa katika makao jirani ya kuwatunza wazee, walihamishwa mara moja. Kulikuwa na ripoti kuwa wazima moto walikuwa wanajaribu kuzima moto wakati mlipuko huo ulipotokea. 
 
 Uharibifu mkubwa ulitokea kwa makao ya kuwahifadhi wazee. Mlipuko ulitokea nyakati za usiku wa kuamkia leo

Zaidi ya watu 100 wamejeruhiwa katika mulipuko uliotokea kwenye kiwanda cha mbolea kilichoko Kaskazini Magharibi mwa eneo la Waco, jimbo la Texas. Wengi wamekwama ndani ya majengo yanayendelea kuteketea kufuatia mulipuko huo.
 
Meya wa Mji kulitokea mulipuko huo, Tummy Muska ameelezea kutokea moto mkubwa uliolipuka sawa na bomu. Mulipuko huo umeharibu majengo ya kiwanda hicho, makaazi ya karibu kikiwemo kituo kimoja cha afya.
Wazima moto, magari ya kubebea wagonjwa na helikopta sita zimetolewa kushughulikia majeruhi na kutuliza hali ya sasa.
 
Majengo kadhaa yameendelea kuteketea karibu na kiwanda hicho cha mbolea.Taarifa ambazo hazijathibitishwa zinasema zinasea kuna watu waliopoteza maisha.
 
Dean Wilson wa idara ya usalama ya Texas amesema nyumba 75 karibu na jengo hilo ziliharibiwa kabisa.
 
Amesema kufikia sasa hawezi kuthibitisha vifo vyovyote. Watu 38 wameripotiwa kua katika hali mahututi. Makundi ya wokozi yameanza kufika nyumba hadi nyingine kuwaokoa majeruhi na kutoa huduma ya kwanza.
 
Kituo cha Dharura kimewekwa kwenye uwanja wa mpira ulioko karibu.Gavana wa Texas amesema afisi yake imetoa raslimali zake kusaidia katika juhudi za wokozi.


  Chanzo: BBC SWAHILI

WATANZANIA WASHINDWA KUFANYA VIZURI KIPINDI CHA TANO CHA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE

01Washindi wa kipindi cha tano cha Guinness Football Challenge Ken Muturi (kushuto) na Chris Mwamgi(kulia) wakishangilia ushindi walioupata huku wakiwa wamebeba pesa taslimu walizojishindia katika shindano hilo jana usiku na pembeni ni mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho Lary Asengo(anayepiga makofi kulia).
 ………………………………………………..
 Jana usiku kupitia Televisheni za ITV na Clouds TV timu ya Tanzania ilishindwa kutumia nafasi ya kipindi cha mwisho cha mashindano ya “Guinness Football Challenge” katika hatua ya Afrika Mashariki baada ya kutolewa na timu kutoka Kenya. Rangi nyekundu imeonekana kuwa ni rangi ya bahati kwa timu za Kenya kwani hii ni timu ya nne kutoka Kenya kufanikiwa kufuzu kuingia hatua ya Pan-African GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGETM. Kenneth Mukuri na Chris Mwamgi ndio walioibuka washindi jana usiku kwani walifanikiwa kufika katika hatua ya mwisho ya kulenga ukuta  wa pesa wa Guinness ambapo walijishindia dola za kimarekani  1,500. 

 Ni vipi Kenneth na Chris wataweza kumudu hatua ya Pan-African? Sasa wana nafasi ya kuiwakilisha nchi yao katika mashindano ya Pan-African ambapo watakutana na wawakilishi pekee kutoka Tanzania, Daniel Msekwa na Mwalimu, washiriki kutoka Uganda Alex Muyobo na Ibrahim Kawoova pamoja na wenzao kutoka Kenya,Francis Ngigi na Kepha Kimani(washindi wa kipindi cha 2), Kenneth Kamau na Wills Ogutu(washindi kipindi cha 3) na Ephantus Nyambura na Samuel Papa(washindi kipindi cha 4).
 Timu hizi tano zitakua uwanjani kutimiza malengo yao, ambapo watakutana uso kwa uso na washiriki kutoka Ghana na Cameroun kuonesha ni nani ana maarifa zaidi na ujuzi wa kusakata kabumbu,  hata kuvishwa ubingwa wa Pan-African na  kuondoka na dola za kimarekani 250,000.
 
 Usikose kuangalia mashindano haya kupitia televisheni za ITV na Clouds TV huku ukiburudika na kinywaji cha GUINNESS.
 
                              Tafadhali kunywa kistaarabu – Hairuhusiwi kwa wenye umri chini ya miaka 18.
Reviewed by crispaseve on 11:22 Rating: 5

No comments

Post AD