NMB YASHIRIKI MAONYESHO BUNGENI
Waziri wa Nchi ya Ofisi ya Waziri mkuu
(Sera,Utaratibu na Bunge)William Lukuvi akipata maelezo kutoka kwa ofisa
wa benki ya NMB Diana Kimaro mara alipotembelea banda la NMB katika
maonyesho yanayoendelea kwenye viwanja vya Bunge.
Mbunge wa Viti Maalum, Mh. Zainabu Vulu
akipata maelezo kutoka kwa Meneja Huduma za Ziada, Alluthe Nungu wakati
walipotembelea banda la NMB.
Baadhi ya maofisa wa benki ya NMB waliopo kwenye maonyesho ya taasisi za kifedha mjini Dodoma.
Ofisa Uhusiano wa NMB, Doris Kilale (wa
pili kushoto) akitoa maeleza kwa mbunge wa viti maalum, Mathew Mlacha na
Mbunge wa Busega, Titus Kamani juu ya
huduma mbambali zinazotolewa na benki ya NMB.
Na Mwandishi Wetu
Na Mwandishi Wetu
Benki ya NMB inashiriki maonyesho ya
huduma za kibenki yanayoendelea katika viwanja vya Bunge mkoani Dodoma.
Lengo la maonyesho hayo ni kuelezea huduma mbali mbali zitolewazo na
benki ya NMB kwa wateja wake.
Reviewed by crispaseve
on
10:44
Rating:
Post a Comment