Header AD

HAFLA YA TUZO ZA WANASOKA BORA TANZANIA WA GAZETI LA MWANASPOTI ILIVYOFANA JANA MLIMANI CITY


Rais wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga kushoto akimkabidhi tuzo ya Ufungaji Bora mshambuliaji wa Azam FC, Kipre Tchetche kutoka Ivory Coast katika tuzo za gazeti la Mwanaspoti usiku wa jana ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam. 

Naibu Waziri wa TEKNOHAMA, Januari Makamba kushoto akimkabidhi tuzo ya Mwanasoka Bora, kiungo wa Yanga SC, Haruna Niyonzima kulia. Anayeshuhudia katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya MCL, Zuhura Muro

Rais wa heshima wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wakili Said El Maamry akimkabidhi tuzo ya Mchezaji bora wa Tanzania anayecheza nje, mwakilishi wa mshindi wa tuzo hiyo, Mbwana Samatta wa TP Mazembe ya DRC.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Geoffrey Nyange 'Kaburu' akimkadhi tuzo Refa Bora, Oden Mbaga

Mshambuliaji wa zamani wa Simba na Yanga, Zamoyoni Mogella akimkabidhi tuzo ya bao bora, mwakilishi wa mshindi wa tuzo hiyo, Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya DRC

Kipa mpya wa Yanga SC, akipokea Tuzo ya 11 Bora kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya MCL, Zuhura Muro kushoto

Amri Kiemba wa Simba SC akipokea tuzo ya 11 Bora

Winga wa Azam FC, Joseph Kimwaga akipokea tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi kutoka kwa Mohammed Rweyemamu, Mjumbe wa Bodi ya MCL 

Mwanahaisi Omar akipokea tuzo ya Mchezaji Bora wa Kike kutoka kwa Makamu Rais wa Shirikisho la Soka la Wanawake (TWFA), Rose Kisiwa kushoto

Makamba akimkabidhi tuzo ya heshima, Nahodha wa zamani wa timu ya soka ya Taifa ya Tanzania, Nicholaus Akwitende kulia 

Nahodha mwingine wa zamani wa Taifa Stars, John Lyimo akipokea tuzo ya heshima kulia

Nahodha mwingine wa zamani wa Taifa Stars, Mbwana Abushiri akipokea tuzo yake

Nahodha mwingine wa zamani Taifa Stars, Omar Zimbwe akipokea tuzo yake ya heshima

Mchezaji wa zamani wa Taifa Stars, Said George aimpokelea tuzo Jellah Mtagwa

Mtangazaji maarufu wa mpira wa zamani wa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD), sasa TBC, Mzee Mshindo Mkeyenge (katikati) akipokea tuzo yake ya heshima

Meneja Uhusiano wa Vodacom, Salum Mwalimu akimkabidhi Tenga tuzo ya Utawala Bora

Wachezaji na wawakilishi wa wachezaji walioteuliwa katika 11 Bora ya gazeti la Mwanaspoti wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kushinda tuzo zao

Mzee King Kiki alitumbuiza 

Rapa Joh Makini akitumbuiaza

Rapa Joh Makini akiwataka waalikwa wainue mikono juu

Na kweli watu wazima waliiua mikono kucheza Hip hop

Rapa Juma Nature akitumbuiza

Ofisa wa Azam FC, Patrick Kahemele akipokea tuzo ya 11 Bora kwa niaba ya Kipre Tchetche

Juma Kaseja na Amri Kiemba baada ya kupokea tuzo zao

Msanii akionyesha utundu na kipaji cha kunyumbulika

Hivi ni vipaji adimu

TBC1 walikuwa live jana

Amerudi Yanga huyu; Kipa wa Coastal Union, Shaaban Kado kushoto akifurahia jambo na kipa mpya wa Yanga SC, Juma Kaseja

Kutoka kulia kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi, kiungo wa Coastal Union, Uhuru Suleiman ma mwigizaji Elizabeth Michael 'Lulu'

Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Ally Mayay kulia akiwa na Kaburu

Ni haki yake kuchoka; Boniface Wambura kulia, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF anafanya kazi sana na haikuwa ajabu aliishia kusinzia kwa uchovu jana wakati wa shetehe za tuzo, kushoto ni Mogella. 
HAFLA YA TUZO ZA WANASOKA BORA TANZANIA WA GAZETI LA MWANASPOTI ILIVYOFANA JANA MLIMANI CITY HAFLA YA TUZO ZA WANASOKA BORA TANZANIA WA GAZETI LA MWANASPOTI ILIVYOFANA JANA MLIMANI CITY Reviewed by crispaseve on 12:02 Rating: 5

No comments

Post AD