Baada ya, Neymar ,sasa, ni ,Van Persie

Hofu kuwa Van Persie huenda asishiriki mechi dhidi ya Argentina
Kocha
wa Uholanzi Lous van Gaal amezua taharuki baada ya kusema kuwa
mashambulizi wake matata van Persie anaugua utumbo na kuwa anahofu iwapo
atacheza dhidi ya Argentika katika mechi ya pili ya nudu fainali au la.
Kocha
Van Gaal amesema kuwa nafasi yake huenda ikachukuliwa na Nigel de Jong
iwapo daktari wa timu hiyo atadhibitisha kuwa van Persie huenda
akashindwa kuhimili uchungu na hivyo kukosa mechi hiyo muhimu.

Je van Persie atacheza dhidi ya Argentina ?
Iwapo
de Jong atacheza basi itakuwa mara yake ya kwanza tangu aondoke uwanjani
katika mechi ambayo Uholanzi iliilaza Mexico mabao 2-1 katika raundi ya
kwanza.
Kocha
huyo anakila sababu ya kuwa na wasiwasi baada ya Nahodha wake
kutoshiriki mazoezi siku ya kuamkia mechi hiyo muhimu , hata hivyo
anaafueni baada ya kurejea kwa Ron Vlaar na Leroy Fer mazoezini.
wawili hao walikuwa wamejeruhiwa katika mechi za makundi.

Argentina inamtegemea Messi kuifungia mabao
Kwa
upande wao Argentina wnaendelea na mazoezi yao kikamilifu ijapokuwa
inatarajiwa kuwa Mshambulizi wa Bracelona Lionell Messi atakabidhiwa
majukumu mahsusi ya kuifikisha Argentina katika fainali yao ya kwanza
tangu mwaka wa 1990.
Argentina
pia wanatatizika kwa kumkosa mchezaji wa kutegemewa Angel Di Maria
ambaye amejeruhi paja lake lakini watakuwa na wasaidizi wake Sergio
Aguero na Marcos Rojo ambao watakuwa kwa ajili ya mechi hiyo ya
kihistoria kwao.
Uholanzi
tofauti na Argentina imefuzu kwa fainali ya kombe la dunia mara mbili
zilizopita ikimaliza ya pili mara mbili mfululizo .Chanzo BBC Swahili
Baada ya, Neymar ,sasa, ni ,Van Persie
Reviewed by crispaseve
on
07:37
Rating:
Post a Comment