Header AD

DKT. ALOYCE NZUKI AFUNGUA WARSHA YA KUKUSANYA MAONI YA WADAU WA KANDA YA KATI KWA AJILI YA KUPITIA UPYA SERA YA TAIFA YA UTALII YA MWAKA 1999 MJINI DODOMA

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha ya siku moja ya kukusanya maoni ya wadau wa sekta ya utalii kwa ajili ya kupitia upya Sera ya Taifa ya Utalii ya mwaka 1999 iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa ushirikiano na Benki ya Dunia na Shirikisho la Utalii Tanzania mjini Dodoma leo. 

Dkt. Nzuki amesema ipo haja sasa kwa Sekta za Umma kuona umuhimu wa kuwekeza moja kwa moja katika biashara ya utalii nchini hususani katika huduma za malazi na usafiri ili kuiwezesha Serikali kupata mapato ya moja kwa moja na kuongeza zaidi kwenye pato la taifa. 

Alisema kwa kuimarisha usafiri wa anga kutawezesha usafiri wa watalii moja kwa moja kutoka kwenye soko na kuwaleta nchini huku wakilipia gharama zote hapa nchini tofauti na hivi sasa ambapo baadhi ya makampuni ya nje hulipwa fedha kiasi nje ya nchi na hivyo kuikosesha Serikali mapato kupitia ushuru unaotozwa na TRA. 

Alisema sio lazima Serikali iwe inasimamia moja kwa moja utoaji wa huduma hizo kwa kuwa upo uwezekano wa kutumia makampuni makubwa hata ya nje ya nchi kuja kuendesha huduma hizo kwa ufanisi zaidi hapa nchini.  
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki (kulia) na wadau wengine wa sekta ya utalii wakimsikiliza Prof. Raphael Mwalyosi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (kulia) wakati akiwasilisha mada kuhusu Hoja ya Marekebisho ya Sera ya Utalii ya Mwaka 1999 katika warsha ya kukusanya maoni ya wadau kwa ajili ya kupitia upya Sera hiyo iliyoandaliwa na Wizara hiyo kwa ushirikiano na Benki ya Dunia na Shirikisho la Utalii mjini Dodoma leo.
Kamu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Deograsias Mdamu akizungumza katika warsha ya siku moja ya kukusanya maoni ya wadau wa sekta ya utalii kwa ajili ya kupitia upya Sera ya Taifa ya Utalii ya mwaka 1999 iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa ushirikiano na Benki ya Dunia na Shirikisho la Utalii Tanzania mjini Dodoma leo. 
Picha ya pamoja ya Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki (katikati waliokaa) na wadau wa sekta ya utalii katika warsha ya siku moja ya kukusanya maoni ya wadau wa sekta ya utalii kwa ajili ya kupitia upya Sera ya Taifa ya Utalii ya mwaka 1999 iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa ushirikiano na Benki ya Dunia na Shirikisho la Utalii Tanzania mjini Dodoma leo.
Baadhi ya wadau wa sekta ya utalii wakisikiliza moja ya mada katika warsha ya kukusanya maoni ya wadau wa sekta hiyo kwa ajili ya kupitia upya Sera ya Taifa ya Utalii ya mwaka 1999 iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa ushirikiano na Benki ya Dunia na Shirikisho la Utalii Tanzania mjini Dodoma leo. 
 Baadhi ya wawezeshaji wa hafla hiyo ambao ni Maafisa Utalii kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii wakisikiliza moja ya mada katika warsha hiyo. 
Baadhi ya wadau wa warsha hiyo wakisikiliza hotuba ya ufunguzi ya Mgeni Rasmi ambaye ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki. 
 Baadhi ya wadau wa warsha hiyo.
Baadhi ya Washiriki wa warsha hiyo kutoka Mikoa ya Kanda ya Kati iliyofanyika mjini Dodoma. (NA HAMZA TEMBA - WIZARA YA MALIASILI NA UTALII)
HOTUBA YA UFUNGUZI YA NAIBU KATIBU MKUU, WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, DKT. ALOYCE NZUKI

HOTUBA YA KAIMU MKURUGENZI IDARA YA UTALII, DEOGRASIAS MDAMU
DKT. ALOYCE NZUKI AFUNGUA WARSHA YA KUKUSANYA MAONI YA WADAU WA KANDA YA KATI KWA AJILI YA KUPITIA UPYA SERA YA TAIFA YA UTALII YA MWAKA 1999 MJINI DODOMA DKT. ALOYCE NZUKI AFUNGUA WARSHA YA KUKUSANYA MAONI YA WADAU WA KANDA YA KATI KWA AJILI YA KUPITIA UPYA SERA YA TAIFA YA UTALII YA MWAKA 1999 MJINI DODOMA Reviewed by crispaseve on 11:17 Rating: 5

No comments

Post AD