Header AD

HAWA NDIO WASANII WATAOSHIRIKI KWENYE KILI MUSIC TOUR 2014

Wasanii wataoshiriki katika Kili TourKilimanjaro premium Lager imeandaa ziara maalumu ya wasanii maarufu kama Kili Music Tour 2014 ni ziara maalum ya wasanii maarufu zaidi ya wasanii maarufu zaidi ya 30 ambao watatoa burudani kwenye mikoa isiyopungua 10 hapa nchini kuanzia Mei hadi Septemba 2014 lengo likiwa ni kupeleka muziki wa Tanzania kwenye kilele cha mafanikio.
Wasanii watakaotoa burudani ni pamoja na Diamond, Ommy Dimpoz, Linex, Proffesor Jay, Izzo Biznes, Kala Jeremiah, Fid Q, Snura, weusi, ben Pol, Mzee Yusuph, Shilole, Mwasiti, Ney wa Mitego, Mwana FA, Khadija Kopa, Juma Nature, Warriors From the East,  Madee, Young Killer, Jambo Squad, AY, Vanessa Mdee, Mashujaa Band, Rich Mavoko na Christian Bella huku Lady Jaydee akitemwa kwenye ziara hiyo licha ya kuchukua Tuzo hizo kwa kile kilichodaiwa kuwa ni Tweet ya dharau aliyomjibu  shabiki aliyekuwa akimtaka awe anahudhuria tuzo hizo .
IMG_2946
Meneja wa bia ya Kilimanjaro George Kavishe akizungumza na waandishi wa habari
Hawa ni baadhi ya wasanii watakaoshiriki katika Kili TourMeneja wa Kili, George Kavishe amesema “Hii ni fursa kwa wasanii kuweza kutambulisha kazi zao katika mikoa hiyo na hatimaye kuongeza fursa kwa mauzo na kukubalika katika mikoa hiyo”.
Pia katika mikoa itakapofanyika tamasha, wasanii chipukizi mikoa hiyo watapewa fursa ya kutumbuiza katika utangulizi. Hii ni kuwajengea uwezo wa kujiamini na pia itakuwa ni jukwaa la kuonyesha vipaji vyao.

Mikoa itakapopita tuzo itakuwa kama ifuatavyo:

Moshi – Mei 24
Mwanza – Mei 31
Kahama – Juni 7
Kigoma – Juni 14
Iringa – Juni 21
Mbeya – Agosti 9
Dodoma – Agosti 16
Tanga – Agost 23
Mtwara – Agosti 30
Dar es Salaam – Septemba 6.
-kililager.com
HAWA NDIO WASANII WATAOSHIRIKI KWENYE KILI MUSIC TOUR 2014 HAWA NDIO WASANII WATAOSHIRIKI KWENYE KILI MUSIC TOUR 2014 Reviewed by crispaseve on 06:28 Rating: 5

No comments