Header AD

HOTEL ZA DOUBLE TREE BY HILTON TANZANIA WADHAMINI SIKU YA CHAKULA ILIYOFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA TANGANYIKA INTERNATIONAL SCHOOLS

 Hotel Za Double Tree By Hilton Tanzania Tarehe 18.10.2014 walidhamini Siku Ya Maonesho Ya chakula Iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Tanganyika International Schools.Akielezea Madhumuni ya kuandaa siku hiyo .

Mkurugenzi wa Mauzo  wa Hotel za Double Tree By Hilton Tanzania Bwana Florenso Kirambata alisema kuwa nia yao kubwa ni kuweza kuyapa fursa makampuni mbali mbali na wajasiliamali wadogo wadogo kuweza kuonyesha uwezo wao na bidhaa wanazotengeneza.

Mr Florenso  akaongeza kuwa zaidi ya wajasiriamali wadogo wadogo 100(mia Moja) na Wakubwa 50(hamsini) walishiriki kwenye maonesho hayo hasa lengo kuu ikiwa ni kuonesha aina mbali mbali za vyakula wanavyozalisha hivyo kuweza kujitangaza na kufahamika.

Pichani Juu Katikati ni Meneja Masoko wa Hotel za Double Tree By Hilton Bwana Florenso Kirambata kushoto ni mpishi mkuu wa Double Tree Hassan na kulia ni Ayman.
 Mpishi Msaidizi wa Hotel ya Double Tree  Awadh(kushoto) Akiwa Anapata maelekezo toka kwa Mpishi mwenzake Ayman namna ya kuandaa na kuchanganya vyakula

  Mpishi mkuu wa Hotel za Double tree Bwana Hassan akitoa maelekezo kwa wasaidizi wake .
HOTEL ZA DOUBLE TREE BY HILTON TANZANIA WADHAMINI SIKU YA CHAKULA ILIYOFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA TANGANYIKA INTERNATIONAL SCHOOLS HOTEL ZA DOUBLE TREE BY HILTON TANZANIA WADHAMINI SIKU YA CHAKULA ILIYOFANYIKA KWENYE VIWANJA VYA TANGANYIKA INTERNATIONAL SCHOOLS Reviewed by crispaseve on 04:26 Rating: 5

No comments

Post AD