JHIKOMAN, ZAWOSE, MAEMBE KUPAMBA ‘KARIBU FESTIVAL’
Msemaji
wa tamasha la Karibu Music Festival, Muslim Nassor ‘Jazzphaa’
(katikati) akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa
utambulisho huo.
..Wapo pia Prof. Jay, Barnaba, Shilole
Na Andrew Chale
WASANII
kutoka ndani na nje wanatarajiwa kupamba tamasha la Muziki la Kimataifa
la ‘Karibu Music Festival’ litakalofanyika kwa siku tatu kwenye mji wa
Kihistoria wa Bagamoyo, Novemba 7 hadi 9 mwaka huu.
Akizungumza
na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika ukumbi wa Idara ya
Habari (MAELEZO) mapema Oktoba 27, Msemaji wa tamasha hilo Muslim
Nassor ‘Jazzphaa’ alisema maandalizi yamekamilika na tayari wasanii
wa awali waliopatikana wapo hadharani wanaendelea na matayarisho huku
akiwaomba watanzania na wadau wa burudani kujitokeza kwa wingi kwenye
tamasha hilo.
Jazzphaa
aliwataka baadhi ya wasanii wa nje na ndani na nchi zao katika mabano
ni Panda (Japan), Maria Kate (Ufaransa), IFE Pianki (Uganda), Masayo
(Japan), Fantuzz (Marekani), Shiwe Musique (Comoro), Dwembede (Kenya) na
Mbiye Ebrima (Guinea).
Mwanamuziki
wa Msafiri Zawose anayepiga nyimbo za Cigogo, akionjesha vionjo vya
moja ya nyimnbo zake kwa wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa
utambulisho kwa wanahabari.
Makundi
na majina ya wasanii kutoka nyumbani ni pamoja na Afrikabisa Band,
Wahapahapa, Segere Original, Jahazi, The Spirit Band na Mama Africa.
Wengine
ni Cocodo Band, Hokororo Band, Swanu Gogo Vibes, Swahili Vibes, Fimbo
Band, Abeneko Music, Man Kifimbo, Saganda na Msafiri Zawose.
JHIKOMAN, ZAWOSE, MAEMBE KUPAMBA ‘KARIBU FESTIVAL’
Reviewed by crispaseve
on
02:16
Rating:

Post a Comment