MSANII SAIDA KALOLE AZUSHIWA KIFO
Jana kumekuwepo na taarifa kutoka kwa mwanahabari, Frederick Katulanda
kupitia kundi pepe la majadiliano la MabadilikoTanzania, zikiipoti kuwa
mwanamuziki aliyekuwa maarufu Tanzania na Afrika Mashariki, Saida
Karoli, amefariki dunia katika ajali ya kuzama kwa boti. Kwamba, boti hiyo iliyokuwa ikisafiri kutoka katika kisiwa cha Goziba ilikumbwa na dhoruba ndani ya maji ya ziwa Nyanza (Victoria) na kusababisha kifo cha mwanamuziki huyo na watu wengine waliokuwa wakisafiri pamoja katika chombo hicho. Taarifa ya Neville Meena imetoa angalizo kutafuta uhakika kwani inasemekana kuwa Saida Karoli ni mzima, yupo jijini Dar es Salaam na hajafariki dunia kama inavyoelezwa: “Nimetafuta namba yake ya simu sijaipata, ila taarifa kutoka Bukoba na ofisi ya Ofisa Utamaduni Muleba zinasema siyo kweli... kulikuwa na uvumi mwingi mjini Bukoba na Wilayani Muleba kuhusu mwanamuziki huyo kufariki lakini baadaye ikathibitika kwamba hakuwa mmoja wa abiria.” ameandika Meena. Kuhusiana na ajali ya boti, Meena amesema, “...ni kweli kwamba kuna boti imezama katika Ziwa Victoria.”ila msanii huyo hakuwepo katika boti hiyo na wala hayupo wilayani Muleba hivyo taarifa hizo hazina ukweli wowote na mtandao huu unamwombea maisha marefu zaidi msanii Saida Kalole |
Reviewed by crispaseve
on
10:14
Rating:
Post a Comment