MWANAMUZIKI H.BABA AFUNGA NDOA NA M’BONGO MOVIE FLORA MVUNGI JIJINI DAR ES SALAAM..
H Baba na mkewe Flora Mvungi katika pozi.
Flora akimnywesha mumewe kinywaji.
H Baba akisaini kitabu cha ndoa.
Baada ya kuvuka mito,milima na mabonde
hatimaye wasanii wa filamu na muziki Bongo Hamis Ramadhan Baba jina la
jukwaa akifahamika kama ‘H. Baba‘ na bi mdada kutoka Bongo Movie Flora
Mvungi weekend hii waliamua wakate vilimi vya watu wanaongea mjini na
kufanikiwa kutimiza ahadi yao ya kufunga ndoa .
Hata ivyo tofauti na watu walivyotarajia
kuhusu sherehe iyo kwamba ingefanyika ukumbini mkali wa staili ya TAKEU
nchini H. Baba alifunguka kuwa aliamua kutokufanya sherehe ukumbini
kutokana na wazee wake kukataa kwani kwa dini ya Kiislamu hairuhusiwi
kufanya sherehe ukumbini ndiyo maana wakaamua kufanya maulidi tu.
Baada ya watu kula na kunywa na maharusi
kusaini vyeti vya ndoa, waliondoka kuelekea nyumbani kwao Mikocheni, Dar
ambako kulikuwa na sherehe ya maulidi kulikokuwa na vyakula na vinywaji
vya kutosha.
Larrybway91 inawapongeza H.Baba na Bi mdada Flora Mvungi na kuwatakia Safari njema katika Ndoa yao
Reviewed by crispaseve
on
08:06
Rating:
Post a Comment