Header AD

PICHA ZA MKOKO MPYA ANAOMILIKI NICK MINAJ.


Rapa Nick minaj  kutoka nchini Marekani  ambaye yupo chini ya Record Label ya Young Money wiki iliyopita aliamu kuonyesha jeuri ya fedha baada ya kuvuta mkoko wa maana aina ya Lamborghini Aventador RoadSter toleo la mwaka 2014 ambapo alisikika akisema kuwa  anampango wa kubadilisha rangi ya gari lake hilo jipya kutoka rangi ya Blue kwenda Pink ambayo ndio rangi aipendayo.
ImagePichani ni gari analomiliki Nick Minaj aina ya Lamborghini AventadorRoadster toleo la mwaka 2014 .
Nick Minaj ni miongoni mwa marapa wa kike duniani walioingia katika listi ya Forbes HipHop King wanaongoza kwa kulipwa mkwanja mrefu  kupitia kazi zake anazofanya za kimuziki na show anazopata pia bi mdada huyo anajishughulisha na kuuza vipodozi vyake kama vile perfume zinazofahamika kwa jina la ‘Pink Friday’ ukichanganya na  dili nono alilopata la kuwa  jaji katika shindano la kutafuta vipaji la American Pop Idol’ ambavyo vyote kwa ujumla vilimfanya aweze kuingiza mkwanja wa kutosha.
PICHA ZA MKOKO MPYA ANAOMILIKI NICK MINAJ. PICHA ZA MKOKO MPYA ANAOMILIKI NICK MINAJ. Reviewed by crispaseve on 12:26 Rating: 5

No comments

Post AD