ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA YAZIDI KUCHANJA MBUGA JIMBO LA BAHI,KESHO KUIVURUGA KONDOA
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji
cha Misisi kata ya Misisi,wilayani Bahi mapema leo,mkoani Dodoma akiwa
ziarani ndani ya jimbo la Bahi.
Ndugu
Kinana amezungumza na wananchi hao waliokuwa wamebeba mabango na kuzuia
msafara wake,kutokana na matatizo yaliyokuwapo katika kijiji hicho na
kukosa ufumbuzi kwa muda mrefu.Wananchi hao walikuwa na lalamiko lao
moja kubwa lililohusu shule yao ya msingi ya Msisi,ambayo madarasa yake
mawili yaliezuliwa paa (kama yaonekanavyo pichani) na mengine kubomoka
kabisa kufuatia mvua kubwa ilionyesha na kusababisha madhara hayo.
Shule
hiyo ya msingi Msisi ilipatwa na dhahma hiyo mnamo mwaka 2011,na mpaka
leo haikuwahi kufanyiwa ukarabati wa aina yoyote huku walimu na
wanafunzi wakipigwa na jua wakati wa masomo.Ndugu Kinana baada ya
kusikiliza lalamiko hilo kutoka kwa wanakijiji hao,alianzisha harambee
ya papo kwa papo iliyohusu viongozi wa CCM mkoa na Wilaya waliokuwa
kwenye msafara huo na kuichangia shule hiyo na kufanikiwa kupata fedha
na vifaa vya ujenzi ambavyo vitapelekea kuanza upya kwa ujenzi wa madara
hayo,Aidha Wananchi wa kijiji hicho walimshukuru Katibu Mkuu wa CCM
Ndugu Kinana kwa harambee alioifanya na kupelekea kupatikana kwa misaada
hiyo.
Mmoja wa wananchi wa kijiji cha Msisi akiwa amebeba bango lake kichwani.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akisoma moja ya bango lililokuwa
limebebwa na mmoja wa wananchi wa kijiji cha Msisi,Wilaya ya Bahi
lililohusu shule ya msingi ya kijiji hicho kukosa madarasa ya kusomea wanafunzi,kufuatia mvua mkubwa kuezua mapaa.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Mh Chiku Galawa
na
Mbunge wa Jimbo la Bahi,Mh Omari Badwel wakishiriki uchimbaji wa
mitaro na kufukia bomba za maji,katika kijiji cha Nguji kata ya Mundemu
wilaya ya Bahi mkoani Dodoma.Mradi huo wa maji unatarajiwa kuhudumia
zaidi ya watu elfu tatu,aidha mradi huo uliogharimu kiasi cha fedha
zaidi ya Milioni mia saba unatarajiwa kukamilika Aprili 15,2015.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipokelewa katika kijiji cha Mundemu wilaya ya Bahi mkoani Dodoma
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na Wananchi wa Bahi mara baada ya
kumaliza kuzungumza na Halmashauri kuu ya Wilaya ya Bahi,ambapo pia Wananchi waliruhusiwa kuuliza maswa na kupatiwa majibu papo kwa papo.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikagua chanzo cha maji (kisima) chenye ujazo wa lita 16 kwa saa,kinachotumia umeme wa jua
Pichani kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishiriki kupalilia majani katika
shamba la mizabibu la Lubala Succoss,katika kata ya Ilindi,wilaya ya Bahi
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndgu Kinana alipokuwa
akizungumza nao jioni ya leo katika kijiji cha kangogo kata ya Babayu,amapo pia alishiriki ujenzi wa nyumba ya waalimu.
Baaddhi
ya Wanahabari wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa
CCM,Ndugu Kinana,uliofanyika katika kijiji cha Chonde,wilaya ya ya Bahi
mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Chonde wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu
Wanachi
wa kijii cha Chonde wakishangilia wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu
Kinana alipokabidhiwa Mkuki na kuvalishwa mgolole ikiwa ni ishara ya
kuwa mmoja wa machifu wa kabila la Wagogo
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiendesha trekta ikiwa ni ishara ya kuzindua mradi
wa matrekta katika
kijiji cha Chonde,Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma jioni ya leo.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akiendesha trekta,wakati
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipozindua mradi huo wa matrekta katika
kijiji cha Chonde,Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma jioni ya leo.
Baadhi
ya wananchi wa kijiji cha Chonde wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu
Kinana alipowahutubia jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara,wilayani
Bahi mkoa wa Dodoma.
ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA YAZIDI KUCHANJA MBUGA JIMBO LA BAHI,KESHO KUIVURUGA KONDOA
Reviewed by crispaseve
on
02:55
Rating:
Post a Comment