Header AD

Serikali, wadau wakutana kujadili mapendekezo ya kulinda na kukuza Haki za Binadamu Nchini




Mkurugenzi Masuala ya Katiba na Haki za Binadamu Kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Sarah Mwaipopo akiongea na wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa matafa, Leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Masuala ya Katiba na Haki za Binadamu Kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Sarah Mwaipopo akiongea na wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakati wa ufunguzi wa kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa matafa, Leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Msaidizi Masuala ya Haki za Binadamu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Nkasori Sarakikya akiongea na wajumbe kutoka Serikalini na Asasi mbalimbali za Kiraia mara baada ya ufunguzi wa kikao cha kujadili mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa matafa, Leo Jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkurugenzi Masuala ya Katiba na Haki za Binadamu Kutoka Ofisi hiyo Bi. Sarah Mwaipopo.
Mjumbe kutoka Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Bi. Blandina Sembu akichangia hoja kwenye eneo la watu wenye ulemavu na masuala ya uandishi wa Habari wakati wa kikao cha kujadili mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa matafa, Leo Jijini Dar es Salaam.

PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO

Serikali,kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali leo imefanya kikao maalumu cha wadau kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali na asasi za kiraia kwa lengo la kuwafahamisha kuhusu kujadiliwa kwa Taarifa ya pili ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya Haki za Binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Period Review).

Vilevile kikao hicho kitatoa fursa ya kujadili kwa kina na kuyapatia misismamo ya awali kama wadau, mapendekezo yaliyotolewa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwa Serikali mnamo mwezi Mei 2016 , na kuainisha sababu ambazo zinafaa kwa mapendekezo yaliyoahirishwa kwa maslahi mapana ya nchi yetu kabla ya kupitishwa rasmi kuwa taarifa ya nchi itakayowasilishwa kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kabla ya terehe 9 Septemba 2016.

Akifungua kikao hicho Mkurugenzi wa masuala ya Katiba na Haki za Binadamu kutoka Ofisi ya Mwansheria Mkuu wa Serikali, Bi Sarah Mwaipopo ameeleza kuwa kikao hicho ni hatua muhimu kkatika mfumo wa maandalizi ya taarifa za usimamizi na utekelezaji wa haki za binadamu nchini ambao umekua ukishirikisha wadau wote kutoka Wizara,Idara na Taasisi za Serikali pamoja na Taasisi zisizo za kiserikali ambapo amesisitiza wadau wote kuendelea kutoa ushirikiano na kutimiza wajibu wao ipasavyo.

“Sote tutambue na kuzingatia kwamba masuala ya haki za biandamu ni mtambuka na kila mtu ana wajibu wa kutekeleza na kuyasemea katika eneo lake”alisema Bi Sarah

Halikadhalika,kwa niaba ya Serikali, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imekua ikiratibu kikamilifu maandalizi na uwasilishwaji wa Taarifa zote za masuala yote ya haki za binadamu kwa kuzingatia mikataba ya Haki za Binadamu ambayo Tanzania imeridhia na utekelezaji wa jukumu hili umeanishwa katika Ibara ya 59(3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 na Sheria ya Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Sura ya 268, kifungu cha 14(f) ambayo ni;

kuratibu masuala ya uaandaaji na utoaji wa taarifa za nchi za utekelezaji wa Mikataba ya Kikanda na Kimataifa ya haki za binadamu amabyo nchi imeridhia ikiwemo masuala yote ambayo yanahitaji utolewaji wa taarifa za aina hiyo na kuziwasilisha kwenye vyombo husika vya Kikanda na Kimataifa kwa ajili ya majadiliano.

Kikao hicho ambacho kitafanyika kuanzia tarehe 30 -31 Septemba 2016 jijini Dar es Salaam kimehudhuriwa na wadau kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambao ni Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Jukwaa la Katiba Tanzania,Chama cha Watu wenye Ualbino Tanzania,MISA-TAN,PINGOS’ FORUM,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa,Wizara ya Katiba na Sheria, Mahakama ya Tanzania,Uhamiaji,Tume ya Haki za Binadamu na utawala bora, Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA), Shrikisho la Watu wenye ulemavu Tanzania( SHIVYAWATA) na Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali. Kwa upande wa Zanzibar ni Wizara ya Kilmo na Mifugo, Wizara za Afya,Mifugo, Kazi,Vijana Wazee,Ofisi ya Mwansheria Mkuu, Jumuia ya Wanawake Wanasheria,Tume ya Uchaguzi

Utaratibu wa Mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Periodic Review) wa masuala ya haki za binadamu ulianzishwa na Umoja wa Mataifa mnamo mwaka 2006 kwa lengo la kuzifanyia mapitio nchi 192 ambazo ni wanachama wa Umoja wa Mataifa, Tanzania ikiwa miongoni, kwa lengo la kuangalia utekelezaji wa masuala ya kulinda na kukuza haki za binadamu nchini mwao.
Serikali, wadau wakutana kujadili mapendekezo ya kulinda na kukuza Haki za Binadamu Nchini Serikali, wadau wakutana kujadili mapendekezo ya kulinda na kukuza Haki za Binadamu Nchini Reviewed by crispaseve on 06:28 Rating: 5

No comments

Post AD