MWAKYEMBE AWAFUNDA WAJUMBE WA KAMATI YA KUZUIA MUAJI YA KIMBARI KWA NCHI ZA MAZIWA MAKUU
Waziri
wa Mambo ya Katiba na Sheria Dkt Harrison Mwakyembe amewataka wajumbe
wa Kamati ya Kimataifa inayojishughulisha na kuzuia mauaji ya kimbari
katika nchi za ukanda wa Maziwa Makuu kuangalia upya mikakati ya kuondoa
vitendo vya mauaji ya kimbari na ukiukwaji wa haki za binadamu katika
ukanda huo.
Dkt.
Mwakyembe amesema Ukanda wa Maziwa Makuu umekuwa ukishuhudia vitendo vya
mauaji ya kimbari vikishamiri licha ya kwamba kila nchi imekuwa
ikichukua jitihada mbalimbali na kusaini makubaliano ya kikanda na
kimataifa ya kuzuia vitendo hivyo.
Amesema
wakati sasa umefika wa kujiangalia ni kwanini vitendo hivyo vimekuwa
vikishamiri pamoja na jitihada zote ambazo kila nchi imekuwa ikizichukua
ili kukomesha vitendo hivyo.
“ Ni
wazi kuwa siku hizi mwelekeo wa matukio ya kihalifu umebadilika,
zimeibuka njia nyingi mpya zinazosababisha mauaji ya kimbari na hata
ukiukwaji wa haki za binadamu, kutokana na hali hiyo kuna haja ya
kuboresha mikakati yenu ili kuzuia kuendelea kutokea kwa mauaji ya
kimbari na ukiukwaji wa haki za binadamu,” alisema.
Aidha
Mhe. Waziri pia amewaambia wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni jukumu lao
kuangalia namna ya kukabiliana changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza
na hivyo kufanya vitendo hivyo kuendelea kuwepo miongoni mwa nchi za
maziwa makuu.Amewataka wataalamu hao kwenda mbali zaidi na kubainisha
hatua zitakazofaa kuchukuliwa za kisera, kisheria na kiutawala ili
kukabiliana na changamoto ya kuendelea kuwepo kwa vitendo hivyo ili
kuvikomesha ndani ya nchi za ukanda wa maziwa makuu
Mhe.
Dkt Mwakyembe alikuwa akifungua mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo
na kubadilisha na uzoefu wajumbe wa Kamati hiyo kwa nchi za Maziwa
Makuu yanayofanyika jijini Dar es salaam. Mafunzo hayo yanajumuisha
wajumbe kutoka nchi za Zambia, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda, Congo
DRC, Sudani Kusini na mwenyeji Tanzania.
MWAKYEMBE AWAFUNDA WAJUMBE WA KAMATI YA KUZUIA MUAJI YA KIMBARI KWA NCHI ZA MAZIWA MAKUU
Reviewed by crispaseve
on
06:01
Rating:
Post a Comment