Header AD

Kampuni ya matangazo ya ADPOLLEX nchini yatoa offer mpya kwa wale wanaotaka kutangaza biashara zao kimataifa





Kampuni ya matangazo ya ADPOLLEX iliyojikita Afrika Mashariki kwenye shughuli za utangazaji sasa imezindua offer mpya ya kukupa nafasi mteja wetu kutangaza biashara/kampuni yako kimataifa kwa sasa kampuni imeaonyesha nia ya dhati ya kuwekeza kwa wajasiriamali wadogowadogo hili kuwazesha wafanyabiashara wadogo kuwekeza kwenye matangazo ili kuongeza mapato yao. Uwekezaji huu unatarajiwa kuongeza tija na muamko wa wafanyakazi na wateja wao.
Kufuatia mabadiliko haya sasa kampuni ya ADPOLLEX  itaweza kuhudumia wateja wake kwa viwango vya juu zaidi huku idadi ya wabunifu na vitendea kazi vikiongezwa.
Akizindua OFFER hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es salaam mwekezaji huyo Bwana CHRISPER MALAMSHA amesema, “nia na madhumini ya uzinduzi huu ni kuitambulisha kampuni hii kwa upya kwa watanzania, licha ya kuwapo hapa nchini kwa zaidi ya miaka miwili.
MALAMSHA aliendelea kusema “soko la Tanzania kwa sasa linakua kwa kasi na sekta ya ushirikiano inazidi kukua kwa viwango vya juu, hivyo umuhimu wa kutangaza masoko na bidhaa zinazozalishwa ni mkubwa mno, kwa kufanya hivi tunatoa nafasi kwa makampuni mengine kutambua uwepo wetu hapa Tanzania na Afrika mashariki na wao kuweza kuzitambua kazi tunazozifanya.
”Kufuatia uwekezaji huu mpya na kukutangazia kampuni yako kimataifa, nia kubwa ni kukuza sekta ya masoko kwa Afrika mashariki huku tukifanya kazi kwenye viwango vya kimataifa. Tunayofuraha kubwa kwa uwekezaji huu kwani utaongeza tija kwa watanzania wenye vipaji.
Kampuni ya ADPOLLEX inatoa huduma mbalimbali kama kuandaa matangazo ya biashara kwa niaba ya wateja, kununua nafasi za matangazo kwenye vyombo vya habari, kuandaa mikakati ya jinsi ya kukuza bidhaa yako, kuwatangazia wateja bidhaa zao kwenye mitandao mbalimbali na kuwashauri hali halisi ya masoko na ushindani ilivyo duniani kwa sasa.
“Ni furaha kubwa kuitambulisha kwenu kampuni ya ADPOLLEX” alisema Bw Daniel Octavian, Meneja Mkuu wa ADPOLLEX Tanzania, huku tukijivunia timu yenye wafanyakazi bora na kazi nzuri ambazo tumeshazifanya mpaka sasa kwa wateja wetu,licha ya kuandaa kazi nzuri zilizoendana na soko la wateja wetu lakini pia tumeonekana kimataifa na kupata nafasi ya kushiriki kwenye baadhi ya forum mbalimbali duniani kwenye sekta ya matangazo. Ushiriki huu utakuwa na manufaa makubwa kwa wateja wetu na kutuwezesha sisi kama ADPOLLEX kupanua wigo wetu wa kufanya kazi kimataifa.
Dhamira yetu ni kuona ushindani wa matangazo ya bidhaa kwa Tanzania unakua na kufikia viwango vya kimataifa.
Bw Daniel aliendeela kusema “Kama kampuni tumefanya kazi hapa Tanzania kwa miaka miwili na makampuni ya ndani na nje ya Tanzania ikiwamo makampuni ya simu, benki, taasisi zisizo za kiserikali,kampuni za samani za ndani, kampuni za sola na nyingine nyingi. Kwa miaka hiyo michache ya kufanya kazi kwa bidii na kutambulika kimataifa,kampuni ya ADPOLLEX sasa inasababu ya kujivunia ujuzi wa kufanya kazi za wazawa huku tukizifanya kwa viwango vya kimataifa. Kama wadau wa matangazo tunaamini ubunifu bora unaleta ushindani katika soko na kuweza kuifikisha bidhaa kwenye viwango vya kimataifa.
Kampuni ya matangazo ya ADPOLLEX nchini yatoa offer mpya kwa wale wanaotaka kutangaza biashara zao kimataifa Kampuni ya matangazo ya ADPOLLEX nchini yatoa offer mpya kwa wale wanaotaka kutangaza biashara zao kimataifa Reviewed by crispaseve on 05:28 Rating: 5

No comments

Post AD