Header AD

MAKOCHA WA SIMBA,ABDALLAH KIBADENI NA JAMHURI KIWEHLO WAFUNGASHIWA VIRAGO,MWENYEKITI RAGE NAYE ASIMAMISHWA

Wakati Kamati ya utendaji ya Simba ikimsimamisha mwenyekiti wake Ismail 


Aden Rage, imewafungashia virago makocha wake Abdallah Kibadeni 'King' na msaidizi wake  Jamhuri Kiwehlo 'Julio' kuinoa timu hiyo yenye maskani yake mtaa wa   Msimbazi.


Akizungumza na Makao Makuu ya klabu hiyo mchana wa leo, Kaimu Mwenyekiti wa Simba Joseph  Itang'are 'Kinesi' alisema kikao cha kamati ya utendaji kilichokaa jana usiku kimefikia uamuzi wa   kumsimamisha mwenyekiti wao kwa kile walichoeleza kutokuwa na imani nae baada ya  kushindwa kuitisha mkutano mkuu wa mabadiliko ya katiba.


Hii itakuwa mara ya pili kwa Rage, kusimamishwa ndani ya klabu hiyo,awali alisimamishwa  mapema mwezi Machi, baada ya wanachama kufanya mapinduzi ya kumuondoa Rage akiwa  kwenye matibabu nchini India hata hivyo aliporudi alisema hatambui mapinduzi hayo na kuitisha   mkutano alioufanya kwenye ukumbi wa Bwalo la Polisi Oyestabay huku akiadi kuitisha  mkutano mkuu wa dharura wa mabadiliko mapema mwezi Agosti hata hivyo aliharisha kwa kile  alichoeleza ni kupisha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Lakini jana Kinesi alisema "Mkutano mkuu wa mwaka ulikuwa ufanyike mwezi huu wa  Novemba na ajenda kubwa ni mabadiko ya katiba, lakini cha kushangaza Rage amewambia  wanachama hakuna mkutano mpaka mwakani na ameondoka yupo nje ya nchi.

"Sasa hii ni ukiukwaji wa katiba, hatuna imani naye na hata kama angekuwepo tungemueleza  wazi kitendo chake hatukiafiki na hatuna imani naye, tumemsimamisha mpaka Desemba Mosi na  hii ni kwa mujibu wa katiba ya Simba kifungu cha 30.

Kinesi alisema Desemba Mosi ndio utafanyika mkutano mkuu wa wanachama na hatma ya Rage 
itajulikana kwenye mkutano huo iwapo wanachama wataridhia kumuondoa au wataamua  adhabu yake ya kumsimamisha iendelee au arejeshwe kundini kumaliza muda wake ambao  unafikia ukingoni Aprili Mwakani.
Mbali na Rage, pia rungu hilo la Kamati ya utendaji limeangukia benchi ya ufundi la klabu hiyo  baada ya kuwafungashia virago Abdallah Kibadeni 'King' na Jamhuri Kiwehlo 'Julio' kutokana 
na mwenendo mbovu wa timu yao iliyomaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi ikiwa inashika  nafasi ya nne ikiwa na pointi 24.


Kinesi alisema nafasi ya Kibadeni itachukuliwa na aliyekuwa kocha wa timu ya Gor Mahia  Zdravko Logarusic raia wa Crotia akisaidiwa na Seleman Matola.
Alisema kocha huyo atatua nchini Desemba Mosi na timu itaanza rasmi mazoezi Desemba 2  kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi.

Kibadeni alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema "Nashukuru nimeacha timu kwenye nafasi  nzuri, kilichofanyika ni demokrasia naheshimu hilo, bado nitaendelea kuwa mwanachama wa  Simba, na bado nina mkataba na klabu hiyo, nitafatilia nipate haki yangu.

CHANZO:MICHUZI BLOG
MAKOCHA WA SIMBA,ABDALLAH KIBADENI NA JAMHURI KIWEHLO WAFUNGASHIWA VIRAGO,MWENYEKITI RAGE NAYE ASIMAMISHWA MAKOCHA WA SIMBA,ABDALLAH KIBADENI NA JAMHURI KIWEHLO WAFUNGASHIWA VIRAGO,MWENYEKITI RAGE NAYE ASIMAMISHWA Reviewed by crispaseve on 12:42 Rating: 5

No comments

Post AD