Samuel Eto'o aifanyia kitu mbaya Man U...apiga 3 Chelsea ikiibamiza Man U 3-1; Tottenham yaichapa Swansea 3-1
Hat-trick
ya Samuel Eto'o imewahakikishia Chelsea kuendelea kutoa shinikizo
katika msimamo katika Premier League huku ikiyadidimiza matumaini ya
Manchester United kuweza kutetea taji lao msimu huu. Mshambuliaji huyo
veteran alifunga mara mbili katika kipindi cha kwanza dakika ya 17 na 49
na akamalizia kazi katika kipindi cha pili baada ya kufunga bao la tatu
dakika ya 49.
Kwa
matokeo hayo sasa Chelsea iko nyuma ya vinara wa ligi hiyo Arsenal kwa
pointi mbili na pointi moja nyuma ya Manchester City wanaoshika nafasi
ya pili kwenye msimamo.
Meneja wa United David Moyes yuko nyuma kwa pointi 14 dhidi ya vinara
Arsenal. Katika mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Stanford Bridge,
Nemanja Vidic alitolewa kwa jadi nyekundu baada ya kumchezea vibaya Eden
Hazard.
Katika mchezo uliopigwa mapema leo, Tottenham iliondoka na pointi tatu
muhimu baada ya kuichapa Swansea 3-1. Mabao ya washindi yamefungwa na
Adebayor dakika ya 35 na 71 na Chico akajifunga dakika ya 53. Bao pekee
la Swansea limefungwa dakika ya 78 na Bony.
Samuel Eto'o aifanyia kitu mbaya Man U...apiga 3 Chelsea ikiibamiza Man U 3-1; Tottenham yaichapa Swansea 3-1
Reviewed by crispaseve
on
12:40
Rating:
Reviewed by crispaseve
on
12:40
Rating:


Post a Comment