KIKUNDI CHA KINAMAMA OFISI YA MKUU WA MKOA RUKWA WATOA MSAADA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA WASIOONA YA MALANGALI MJINI SUMBAWANGA
Mwalimu
Mkuu wa Shule ya Msingi ya Wasioona Malangali Mwl. Orthor M. Mkangara
akitoa maelezo mafupi ya shule hiyo iliyoanzishwa rasmi mwaka 1998
ambapo mpaka hivi sasa ina jumla ya wanafunzi 71 wengi wao wakiwa
wasioona na baadhi wakiwa ni walemavu wa ngozi "Albinism". Alisema kwa
sasa shule hiyo inahitajio kubwa na vifaa vya kufundishia pamoja na
usafiri kwa ajili ya kurahisisha shughuli mbalimbali shuleni hapo.
Alisema kuwa zipo changamoto nyingi shuleni hapo ambapo wadau mbalimbali wanakaribishwa katika kusaidia kuzitatua. Aliwashukuru kikundi cha kinamama kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa (pichani kushoto) kwa msaada waliotoa na kuomba wadau wengine kuwa na moyo kama huo katika kusaidia watoto wenye ulemavu hapa nchini.
Alisema kuwa zipo changamoto nyingi shuleni hapo ambapo wadau mbalimbali wanakaribishwa katika kusaidia kuzitatua. Aliwashukuru kikundi cha kinamama kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa (pichani kushoto) kwa msaada waliotoa na kuomba wadau wengine kuwa na moyo kama huo katika kusaidia watoto wenye ulemavu hapa nchini.
Katibu
wa Kikundi cha Kinamama Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa Bi. Joyce
Mwanandenje akizungumza kwa niaba ya umoja huo ambapo alisema lengo la
ujio wao Shuleni hapo ni kutimiza desturi yao ya kila mwaka ambapo
hutembelea makundi ya wahitaji mbalimbali katika kuadhimisha siku ya
wanawake duniani. Katika salam zao shuleni hapo walitoa msaada wa
magodoro 20, Sukari, sabubi na zawadi mbalimbali kwa aijili ya
wanafunzi. Kikundi hicho cha Kinamama Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa
kinaundwa na watumishi wanawake kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Hazina
Ndogo, Ukaguzi wa Ndani, Chuo Kikuu Huria na Baraza la Nyumba na Ardhi
Mkoa.
Baadhi
ya wanafunzi shuleni hapo wakiimba wimbo mwanana wa kuwakaribisha
kikundi cha kinamama Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa walipofika shuleni
hapo.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
KIKUNDI CHA KINAMAMA OFISI YA MKUU WA MKOA RUKWA WATOA MSAADA KWA WANAFUNZI WA SHULE YA WASIOONA YA MALANGALI MJINI SUMBAWANGA
Reviewed by crispaseve
on
00:16
Rating:
Reviewed by crispaseve
on
00:16
Rating:




Post a Comment