Header AD

MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHIWA CHETI CHA ULEZI WA HIARI WA CHAMA CHA WENZA WA MABALOZI WA AFRIKA WALIOKO UBELGIJI


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea cheti maalum cha ulezi wa heshima wa Chama cha wenza wa mabalozi wa nchi za Afrika walioko nchini Ubelgiji (Honory Patronese of the Association of the Spouses of African Ambassadors in Belgium) kutoka kwa Mke wa Balozi wa Cameroon nchini Ubelgiji Mama Christiane Eloundov de Evina wakati wa chakula cha mchana walichowaandalia wake wa Marais wa Afrika jijini Brussels tarehe 2.4.2014.
Mke wa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Mama Adelaida Kamala akimkabidhi Cheti Maalum cha ulezi wa heshima cha wenza wa mabalozi wa Afrika walioko Ubelgiji, Mke wa Rais wa Cameroon Mama Chantal Biya wakati wa chakula cha mchana walichowaandalia wageni hao kwenye hoteli ya Sheraton tarehe 2.4.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wake wa Marais na Wakuu wa nchi za Afrika pamoja wa wenza wa Mabalozi wa nchi hizo mara baada ya kupata chakula cha mchana kilichoandaliwa na wenza hao tarehe 2.4.2014. 
MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHIWA CHETI CHA ULEZI WA HIARI WA CHAMA CHA WENZA WA MABALOZI WA AFRIKA WALIOKO UBELGIJI MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHIWA CHETI CHA ULEZI WA HIARI WA CHAMA CHA WENZA WA MABALOZI WA AFRIKA WALIOKO UBELGIJI Reviewed by crispaseve on 15:17 Rating: 5

No comments

Post AD