Header AD

TAARIFA YA MELI YA MIZIGO ILIYOZAMA ZIWA VICTORIA


Watu 10 wamenusurika kufa maji katika ziwa 
Victoria baada ya meli ya mizigo Fb Matara 
 
kupinduka na kuzama ikiwa na shehena ya sukari 
tani 280 zilizonunuliwa katika kiwanda cha sukari 
 
Kagera wakati ikitoka Bukoba kwenda jijini

Mwanza.
Meli hiyo inayomilikiwa na kampuni ya Mkombozi 
 
fishing and marine transport limited, imezama 
ikiwa na magunia 5600 ya sukari sawa na tani
 
280, mali ya mfanyabiashara wa jijini Mwanza 
aitw ye V.h.Shah, ambapo mkurugenzi wa 
kampuni hiyo Gitano Chacha Munanka ameeleza
 
kwamba meli hiyo imezama ikiwa katikati ya visiwa
vya Kerebe na Lukolu majira ya saa 10.30 usiku 
na kuongeza kwamba hakuna mtu yeyote
 
aliyejeruhiwa kufuatia tukio hilo. 
ITV imeshuhudia meli hiyo ikiwa imepinduka huku juhudi za wafanyakazi wa kampuni hiyo kuipundua
zikiwa zinaendelea bila mafanikio, huku baadhi yamashuhuda wa tukio hilo wakisema chanzo cha meli hiyo kuzama ni kutokana na dhoruba kali
ambapo wametoa ushauri kwa wamiliki wa vyombo vya majini kuzingatia utabiri unaotolewa na mamlaka ya hali ya hewa nchini ili kuepusha
maafa.

Meli hii inayoonekana pichani ni mfano wa meli iliyozama,ambayo ilianza safari yake ya kutoka Bukoba majira ya saa 7 mchana, ikiwa inaendeshwa na kapteni Erick Lasan  mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi kavu
Sumatra kanda ya ziwa, umethibitisha kuzama kwa meli hiyo yenye uwezo wa kubeba tani 280 za mizigo na abiria 100.

Chanzo ITV
TAARIFA YA MELI YA MIZIGO ILIYOZAMA ZIWA VICTORIA TAARIFA YA MELI YA MIZIGO ILIYOZAMA ZIWA VICTORIA Reviewed by crispaseve on 05:41 Rating: 5

No comments

Post AD