Header AD

YOUNG JEEZY MIKONONI MWA POLISI KWA KUKUTWA NA BUNDUKI


2012 BET Awards - Arrivals
Rapa mzaliwa wa Atlanta nchini Marekani, Jay Jankins AKA Young Jeezy amekamatwa na polisi kwa madai ya kukutwa na bunduki baada ya mtu mmoja kufariki Dunia kwa kupigwa risasi kwenye Tamasha la muziki la Wiz Khalifa lililofanyika Mountain View mjini California.
Tukio hilo lilitokea usiku wa Agosti 22   ambapo mtu huyo aliyetambulika kwa jina la Eric Johnson mwenye miaka 38 alifyetuliwa risasi tatu mfululizo akiwa backstage na baadae kufariki Dunia hospitalini.
Inaelezwa kwamba jumapili iliyopita(Agosti24) polisi walifanikiwa kukuta bunduki aina ya Rifle ikiwa ndani ya basi la Young Jeezy waliyoamini kuwa ni yake na hivyo kuwalazimu kuwatia nguvuni wapambe wake pia.
Kwa mujibu wa mtandao wa E! Online umeripoti kwamba watu wengine waliokamatwa ni pamoja na Kena Marshall, Peter Maynard, David Kuniansky-Altman, William Gilmore, na Alexa Beason huku dhamana ya Jeezy ikiwa dola za kimarekani milioni moja.
YOUNG JEEZY MIKONONI MWA POLISI KWA KUKUTWA NA BUNDUKI YOUNG JEEZY MIKONONI MWA POLISI KWA KUKUTWA NA BUNDUKI Reviewed by crispaseve on 06:40 Rating: 5

No comments

Post AD