JAJI : OSCAR PISTORIUS HAKUUA KWA KUKUSUDIA
Oscar Pistorius akiwa kizimbani
Jaji anayetoa uamuzi katika kesi ya mauaji inayomkabili
mwanariadha wa mbio za Paralyimpiki, Oscar Pistorius amesema upande wa
mashtaka umekosa kuthibitisha kikamilifu shtaka kuu la kwanza dhidi ya
Pistoriuos kuwa alikusudia kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp
Hata hivyo jaji huyo Thokozile Masipa amepinga ushahidi wa
upande wa utetezi kwamba mwanariadha huyo hakunuwia kutenda uhalifu huo
alipomuua mpenzi wake River.
Pistorius alikiri kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp nyumbani
kwake mwaka jana katika siku ya wapendanao lakini amekana kumuua kwa
makusudi na kusema alidhani mwizi amevamia nyumba.
Kwa upande wa mashtaka unasisitiza kuwa Pistorius alimuua
Reeva kwa makusudi baada ya wapenzi hao wawili kutofautiana huku taarifa
zaidi zikidai kuwa Jaji Thokozile Masipa huenda akachukua hadi Ijumaa
yaani kesho kumaliza uamuzi wake.
Pistorius huenda huenda akafungwa jela miaka 25 kama atapatikana na hatia ya kumuua mpenzi wake.
JAJI : OSCAR PISTORIUS HAKUUA KWA KUKUSUDIA
Reviewed by crispaseve
on
01:19
Rating:

Post a Comment