PENZI LA FRENCH MONTANA NA KHLOE KARDASHIAN IMEBAKI STORI
French Montana na Khloe Kardashian
Trouble In Paradise!!! Baada ya kudumu kwenye mahusiano ya
kimapenzi ya nguvu ya soda kwa takribani miezi 8, Rapa mwenye asili ya
Morocco, French Montana amepigwa chini na mrembo Khloe Kardashian kwa
amani huku kila mmoja akiongea lake.
Kwa mujibu wa habari zilizotanda kwenye mitandaoni mingi ya
udaku zinadai ya kwamba Montana amekuwa tegemezi na kumtumia kimaslahi
mpenzi wake huyo ambaye ni staa wa kipindi cha televisheni cha Keeping up with the Kardashian.
Siku chache zilizopita Khloe aliposti ujumbe mzito kwenye
ukurasa wake wa Instagram uliotafsiriwa kama dongo kwa Montana ambaye
katika kipindi cha mapenzi yao motomoto aliwahi kumzawadia mkoko aina ya
Jeep kwenye siku yake ya kuzaliwa.
”maybe one day we’ll find that place where you and i could be
together. and we’ll catch our dreams. so smile for me one last time and
believe that we’ll meet again. until then, i ‘ll be missing you”. aliandika Khloe
Awali Khloe anayetokea kwenye familia ya Kardashians alikuwa
mke wa mcheza kikapu Lamar Odom kabla ya kuamua kutalikiana kishingo
upande mwaka jana kwa kile kilichotajwa kuwa ni usaliti na matumizi ya
madawa ya kulevya.
PENZI LA FRENCH MONTANA NA KHLOE KARDASHIAN IMEBAKI STORI
Reviewed by crispaseve
on
01:16
Rating:

Post a Comment