YANGA YATWAA NGAO YA JAMII KWA KUITANDIKA BAO 3 – 0 AZAM FC
Kikosi cha Yanga
Wakali ya Jangwani, kikosi cha Yanga kimefanikiwa kutwaa ngao
ya jamii baada ya kuwapa kichapo cha magoli 3 – 0 wanalambalamba wa
Azam Fc katika mchezo uliochezwa Jumapili ya Septemba 14 katika uwanja
wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Brazil, Geilson
Santos ”Jaja” aliweza kuipatia Yanga mabao mawili mnamo dakika ya 58′ na
66′ kabla ya Simon Mvuva kukamilisha karamu hiyo ya magoli kwa
kutupia bao la tatu mnamo dakika ya 88 na mchezo kumalizika kwa Yanga
kutwaa Ngao ya Jamii.
Mara baada ya mchezo huo kocha mkuu wa Young Africans
mbrazili Marcio Maximo alisema anawashukuru wachezaji wake kwa kucheza
kwa kufuata maelekezo yake hali iliyoplekea kucheza soka safi la
kuburudisha linaloambatana na ushindi.
Aidha Maximo alisema baada ya ushindi wa leo maandaliz ya mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar yataanza siku ya jumanne ambapo kwa kesho ametoa mapumziko kwa wachezaji wote pamoja na benchi la Ufundi.
YANGA YATWAA NGAO YA JAMII KWA KUITANDIKA BAO 3 – 0 AZAM FC
Reviewed by crispaseve
on
03:55
Rating:

Post a Comment