LUDACRIS AMCHUMBIA MPENZI WAKE KWENYE NDEGE

Luda na mpenzi wake Eudoxie
Rapa Ludacris ameamua kufanya kweli baada ya kumchumbia
mpenzi wake aliyedumu nae kwa kipindi kirefu aitwae Eudoxie wakati
wakiwa kwenye ndege ya kukodi wakielekea nchini Costa Rica kwa ajili ya
mapumziko mafupi ya Christmas na Mwaka mpya
Kama sehemu ya ombi, Luda alimsapraiz mpenzi wake kwa
kumuonyesha maneno yaliyoandikwa ”Eudoxie, will you marry me? wakati
ndege yao ikiruka juu ya eneo hilo, tukio lililoshuhudiwa na marafiki
zao wa karibu Monica na Shannon Brown..
”She didn’t say yes. She said HELL YES! #milehighproposal” aliandika Ludacris kwenye ukurasa wake rasmi wa twitter.

Baada ya Luda kumsapraiz mpenzi wake

Ludacris na marafiki zake wa karibu baada ya kutua nchini Costa Rica
LUDACRIS AMCHUMBIA MPENZI WAKE KWENYE NDEGE
Reviewed by crispaseve
on
10:28
Rating:

Post a Comment