PATCHO MWAMBA : SIJAFUMANIWA NA MKE WA MTU NI ALEJI YA MACHO TU!

Pichani ni Patcho mwamba Kabla na baada ya kupata kasumba hiyo
Mwanamuziki wa Bendi ya wazee wa Ngwasuma Fm Academia na
mwigizaji wa Bongo Movie, Patcho Mwamba amekanusha vikali habari
zilizozagaa kwenye mitandao na media mbalimbali akidaiwa kuchezea
kichapo baada ya kufumaniwa na mke wa mtu eneo la Kinondoni Jijini Dar
es salaam.
Kwa mujibu wa tovuti ya Global Publishers ilimnukuu Patcho
akisema picha iliyozagaa mitandaoni ikimuonyesha ameumuka usoni ni yeye
mwenyewe aliamua kuisambaza baada ya kupata aleji ya macho kutokana na
kunywa pombe.
”Unajua nina aleji na pombe pamoja na vumbi, nikitumia tu pombe lazima macho yangu yavimbe” alisema Patcho na kuongeza, ”juzi
nilikunywa Windhoek mbili na usiku hali yangu ikabadilika na macho
kuvimba, baada ya tukio hilo niliamua kujipiga picha na kuipost katika
mtandao wa Instagram na hapo ndipo balaa likazuka”.
PATCHO MWAMBA : SIJAFUMANIWA NA MKE WA MTU NI ALEJI YA MACHO TU!
Reviewed by crispaseve
on
10:26
Rating:

Post a Comment