Header AD

IKULU YA MAREKANI YAMSAKA ALIYEVUJISHA SELFIE YA MTOTO WA RAIS OBAMA MTANDAONI


Baada ya kuzagaa kwa habari juu ya kuvuja kwa picha aina ya selfie kwenye mtandao wa Twitter kupitia akaunti ya Masked Gorilla ambayo alipiga mtoto wa Rais wa Marekani, Barack Obama, Malia Obama ikimuonyesha akiwa amevaa Tshirt ya Pro Era ambayo ni brand ya rapa maarufu wa Brooklyn, Joey Bada$$ imepelekea ikulu ya Marekani kuanzisha uchunguzi ili kuweza kubaini mtu aliyevujisha picha hiyo.
Malia Obama
Malia Obama akiwa ametupia kitu cha Pro Era
Kwa mujibu wa Fox News imeripoti kwamba ikulu ya Marekani inaangalia ni jinsi gani selfie hiyo ilivujishwa kwenye mtandao kwa mara ya kwanza huku  watu wakiwa hawana uhakika wa asilimia 100 kama picha hiyo ni ya kweli.
Michelle Obama ameweka sheria kali kwa binti zake kujihusisha na mitandao ya kijamii na huenda akawa hajapendezwa kabisa na kitendo cha picha iyo ya binti yake kutumika kwenye blogu za Rap na kupigia debe brand hiyo.
”Mimi bado  si muhumini mkubwa wa Facebook kwa matumizi ya vijana wadogo”, alisema Michelle wakati akihojiwa na mtangazaji Barbara Walters akielezea jinsi alivyowadhibiti mabinti zake, Malia na Sasha kujihusisha na mitandao ya kijamii.
IKULU YA MAREKANI YAMSAKA ALIYEVUJISHA SELFIE YA MTOTO WA RAIS OBAMA MTANDAONI IKULU YA MAREKANI YAMSAKA ALIYEVUJISHA SELFIE YA MTOTO WA RAIS OBAMA MTANDAONI Reviewed by crispaseve on 02:38 Rating: 5

No comments

Post AD