Header AD

MAN CITY YAMUONGEZEA MKATABA FRANK LAMPARD HADI MWISHO WA MSIMU

Frank Lampard
Hatimaye Klabu ya Manchester City imemuongezea mkataba kiungo mkongwe Frank Lampard hadi mwisho wa msimu wa ligi kuu.
Lampard mwenye miaka 36 amemaliza mkataba wake na klabu ya New York City ya Marekani usiku wa kuamikia leo kwa maana iyo atabakia Etihad hadi mwisho wa msimu na atakosa mechi za mwanzo za ligi kuu ya Marekani ‘Major League’ au MLS.
Klabu ya New York City ilimsaini Lampard mara baada ya kuachwa na Chelsea ya England Juni mwaka jana na klabu ya Manchester City kumuomba kurejea ili acheze kwa mkopo kwa kuwa ligi ya marekani inaanza March mwaka huu.
Kuongezewa mkataba kwa Lampard kumekuwa ni faraja kubwa kwa kocha Emmanuel Pellegrini kwa kuwa atakuwa mbadala wa kiungo Yaya Toure anayejiunga na timu yake ya Taifa Ivory Coast kuanzia January, 05 katika fainali za Afrika nchini Guinnea ya ‘GuinneEquator.
Lampard amekishwa ichezea Manchester City mechi 17 akiwa ameweka wavuni mabao 6 huku akitajwa kuwepo katika kikosi cha leo kitakachovaana na timu ya Sunderland kwenye uwanja wa Etihad.
MAN CITY YAMUONGEZEA MKATABA FRANK LAMPARD HADI MWISHO WA MSIMU MAN CITY YAMUONGEZEA MKATABA FRANK LAMPARD HADI MWISHO WA MSIMU Reviewed by crispaseve on 23:00 Rating: 5

No comments

Post AD