Header AD

RICK ROSS AONYESHA MAPENZI KWA MIAMI HEAT BAADA YA KUCHORA TATTOO HII

Rapa na C.E.O wa lebo ya Maybach Music Group, Rick Ross ameonyesha mapenzi ya hali ya juu kwa timu ya mpira wa kikapu ya Miami Heat inayoshirki ligi kuu ya NBA baada ya kuchora tattoo mpya usoni kwake yenye nembo ya timu hiyo.
Rick Ross
Rick Ross akionyesha Tattoo mbili mpya ambazo amechora usoni ikiwemo nembo ya Miami Heat na Dream Chasers ‘DC’.
Rick Ross alikuwa ameongozana na lebo mate wake Meek Mill ambaye pia alichora nembo ya MMG kwenye kiganja cha mkono wake zoezi lililofanywa na duka la Unroyal Ink ambao ni wataalam wa uchoraji Tattoo.
Mapema katika msimu mpya wa ligi ya NBA, Ross alifanya uwekezaji mwingine mkubwa katika timu ya Miami baada ya kuiwekea dola 10,000 za kimarekani kama sehemu ya kuitabiria kumaliza msimu na rekodi nzuri kuliko Cleveland Cavaliers, kufuatia Lebron James kuhamia kwenye timu iyo akitokea kwao.
RR
Rick Ross akichorwa tattoo huku mkononi akiwa ameshika sigara kubwa
Rick Rozzay
Rozzay akionyesha Tattoo nyingine alizochora hapo awali
Meek Mill Tat
Meek Mill akionyesha Tattoo ya MMG ambayo amechora kwenye kiganja cha mkono wake
Meek Mill DC
                       Meek Mill na Rick Rozzay       wakiwa wameunganisha mikono yao ikiwa ni ishara ya kusapotiana kwa kuchora Tattoo yenye logo ya mwenzake – MMG na DC for Life.
RICK ROSS AONYESHA MAPENZI KWA MIAMI HEAT BAADA YA KUCHORA TATTOO HII RICK ROSS AONYESHA MAPENZI KWA MIAMI HEAT BAADA YA KUCHORA TATTOO HII Reviewed by crispaseve on 23:29 Rating: 5

No comments

Post AD