MFUMUKO WA BEI WAONGEZEKA KIDOGO KUTOKA ASILIMIA 4.0 MWEZI JANUARI, 2015 HADI KUFIKIA ASILIMIA 4.2 MWEZI FEBRUARI, 2015.

Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za
Jamii Epraim Kwesigabo kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) akizungumza na
Waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya
kuongezeka kwa Mfumuko wa Bei nchini kwa mwezi Februari, 2015. Kulia kwake ni
Kaimu Meneja wa Takwimu za Ajira na Bei wa Ofisi hiyo Bi. Ruth Minja.

Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa
kazini wakati Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Epraim
Kwesigabo kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu akizungumza nao leo jijini Dar es
Salaam kuhusu taarifa ya kuongezeka kwa Mfumuko wa Bei nchini kwa mwezi
Februari, 2015. (PICHA ZOTE NA VERONICA
KAZIMOTO)
======== ====== =========
MFUMUKO
WA BEI WAONGEZEKA KIDOGO KUTOKA ASILIMIA 4.0 MWEZI JANUARI, 2015 HADI KUFIKIA
ASILIMIA 4.2 MWEZI FEBRUARI, 2015.
Na:
Veronica Kazimoto,
Dar
es Salaam,
09
Machi, 2015.
Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Februari, 2015
umeongezeka kwa asilimia 4.2 kutoka
asilimia 4.0 mwezi Januari mwaka 2015.
Hayo yamesemwa leo na
Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Epraim Kwesigabo kutoka Ofisi ya Taifa
ya Takwimu (NBS) ambapo amesema kuwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na
huduma kwa mwaka ulioishia mwezi Februari, 2015 imeongezeka kidogo ikilinganishwa
na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia mwezi Januari, 2015.
“Kuongezeka kwa Mfumuko
wa Bei wa mwezi Februari, 2015 kumechangiwa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya
bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Februari,
2015 zikilinganishwa na bei za mwezi Februari, 2014, amesema Kwesigabo”.
MFUMUKO WA BEI WAONGEZEKA KIDOGO KUTOKA ASILIMIA 4.0 MWEZI JANUARI, 2015 HADI KUFIKIA ASILIMIA 4.2 MWEZI FEBRUARI, 2015.
Reviewed by crispaseve
on
07:46
Rating:
Reviewed by crispaseve
on
07:46
Rating:

Post a Comment