Watanzania kunufaika zaidi na Gesi Asilia
·
Iwapo kutakuwepo ushirikishwaji wa wananchi
· Wataalamu nao watoa yao ya moyoni
Dar es salaam, Jumatatu Aprili 24, 2015 --KUTOKANA na kugundulika kwa hazina
kubwa ya gesi nchini ambayo inategemewa kukuza pato la taifa zaidi ya
mara 15 ya sasa, kiasi cha kuiwezesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zenye
uchumi wa kati kufikia mwaka 2025.
Hata hivyo, dhana ya kwamba Rais ajaye baada ya uongozi wa
Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete kumaliza muda wake, anaweza akaikuta Tanzania
ikiwa ni nchi tajiri tayari kutokana na rasilimali hiyo ya gesi asili, inaweza
isiwe sahihi kama hautawekwa mfumo madhubuti wa ushirikishwaji wa wananchi katika
fursa zilizopo katika rasilimali hiyo, sera, sheria na usimamiaji mzuri wa
raslimali hiyo.
Pia itawezekana tu iwapo viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia
rasilimali hiyo watahakikisha wanaisimamia kikamilifu kwa mujibu wa sera na
sheria zitakazotungwa na kusimamiwa na viongozi wenye dhamira ya dhati ya
kuwatumikia Watanzania na nchi yao kwanza.
Hayo pamoja na mengine yalijadiliwa hivi karibuni jijini Dar es
Salaam na Watanzania wapatao 400 kutoka wilaya mbalimbali ambapo walitoa maoni
yao kuhusu ni jinsi gani mapato yatakayotokana na gesi yatawanufaisha wananchi
wote wa Tanzania.
Mkutano huo uliowakutanisha Watanzania na kuwawezesha kutoa
mawazo na maoni yao kama wawakilishi wa maeneo watokayo uliandaliwa na taasisi
za utafiti kuhusiana na kuondokana na umaskini nchini za REPOA na
Center for Global Development (CGD).

Dr Abel Kinyondo & Invited Expert Innocent Bash from TEITI addressing the media

Dr Abel Kinyondo Opening Speech .
+answering+questions.jpg)
Expert Mr Dennis Rweyemamu (Head - Policy and Research, UONGOZI INSTITUTE) answering questions

January Makamba and Mujobu Moyo listening to participants

January Makamba answering questions from participants

Moderator discussing topics with participants
Watanzania kunufaika zaidi na Gesi Asilia
Reviewed by crispaseve
on
02:59
Rating:
Reviewed by crispaseve
on
02:59
Rating:

Post a Comment