Header AD

BONDIA CHEKA KUPANDA ULINGONI MEI 30 P.T.A SABASABA JIJINI DAR KUZICHAPA NA MTHAILAND

BONDIA Fransic Cheka atapanda ulingoni kwa mara ya kwanza kabisa baada ya kutoka jela, ambapo atacheza na Kiatchai Singwancha  kutoka 


nchini Thailand ,mpambano huo wa raundi 10 utafanyika katika ukumbi wa P.T.A Sabasaba jijini Dar es salaam,

Akizungumza matayarisho ya mpambano  huo, promota Kaike Siraju amesema kuwa amejipanga vizuri kwani kila kitu kinaenda sawa kwa hivi sasa, ambapo mabondia wa utangulizi wote wanatarajia kusainishwa wiki hii.

Mpambano huo utakaosimamiwa na chama cha ngumi za kulipwa nchini P.ST chini ya rais wake Emanuel Mlundwa

Wamesema kuwa wao wako tayari kwa mpambano huo na bondia wa Thailand ataingia nchini siku tatu kabla ya mpambano huo,ambao utavuta hisia za wapenzi wengi wa mchezo wa ndondi nchini

siku hiyo  Vicent Mbilinyi 'Sugu'  atavaana na  Keis Amal 

Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi  kali pamoja na kutambua sheria zake zikiwa na mabondia wakali kama vile
Floyd Mayweathar,Manny Paquaio, Saul 'canelo' alverez ,Mike Tyson,Mohamed Ali,Ferex Trinidad,Miguel Cotto na wengine wengi,pia kuta kuwa na vifaa vya mchezo vitakaokuwa vikitolewa na Rajabu Mhamila 'Super D' kwa mabondia watakaofanya vizuri siku hiyo na vingine kuuzwa kwa pesa taslimu na kocha huyo kwa ajili ya kuamasisha
BONDIA CHEKA KUPANDA ULINGONI MEI 30 P.T.A SABASABA JIJINI DAR KUZICHAPA NA MTHAILAND BONDIA CHEKA KUPANDA ULINGONI MEI 30 P.T.A SABASABA JIJINI DAR KUZICHAPA NA MTHAILAND Reviewed by crispaseve on 05:38 Rating: 5

No comments

Post AD