UMOJA WA MATAIFA WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA
Rais 
wa IRMCT, Bw. Theodor Meron akiwasilisha mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa
 Mataifa, hapo siku ya jumatano, Ripoti ya utendaji kazi wa Matawi ya 
Mahakama za Kimataifa za Kesi za Masalia zinachokua nafasi ya iliyokuwa 
Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR) na Mauaji 
ya halaiki yaliyotokea katika iliyokuwa Yugoslavia ya zamani ( ICTY. Bw.
 Meron alitumia pia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa 
ushirikiano wa hali na mali katika ujenzi wa majengo yanayochokua nafasi
 ya ICTR majengo hayo yamejengwa katika eneo la Lakilaki Mkoani Arusha.
.Mwakilishi
 wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi akizungumza 
wakati wa uwasilishwaji wa Ripoti ya utendaji kazi wa IRMCT ambapo 
alimshukuru kwa namna ya pekee Msajili wa IRMCT Bw. John Hopkins kwa 
uongozi wake na ushirikiano ambao ameonyesha katika ujenzi wa majengo 
mapya huko Lakilaki lakini pia katika kusimamia kipindi cha mpito na 
makabidhiano kutoka ICTR kwenda IRMCT.
Na Mwandishi Maalum, New York
Umoja 
wa Mataifa kwa mara nyingine tena, umeishukuru Serikali ya Tanzania kwa 
kusaidia kwa hali na mali ujenzi na hatimaye kuelekea ukamilishwaji wa 
Majengo mapya ambayo yatatumika kwa shughuli za iliyokuwa Mahakama ya 
Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ( ICTR) ambayo ilihitimisha 
majukumu yake mwaka jana.
Shukrani
 hizo zimetolewa siku ya jumatano na Bw.Theodor Meron, ambaye ni Rais wa
 Mahakama za Kimataifa za Kesi za Masalia na Utunzaji wa kumbukumbu na 
nyaraka zote muhimu za zilizokuwa Mahakama za Kimataifa 
zilizoshughulikia mauaji ya halaiki yaliyotokea Rwanda na Yugoslavia ya 
zamani ( IRMCT).
Bw. 
Theodor Meron alikuwa akiwasilisha Ripoti yake ya Nne kuhusu IRMCT mbele
 ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa . Ripoti ambayo imeanisha maendeleo 
ya kipindi cha mpito kutoka ICTR na ICTY kwenda IRMCT kazi ambayo 
amesema inakwenda vizuri ingawa kumekuwapo na changamoto kadhaa.
“Wakati
 ninapowasilisha ripoti hii, nichukue fursa hii kutoa shukrani zangu za 
dhati kabisa kwa mchango mkubwa na ushirikiano ambao tumeupata kutoka 
serikali ya Tanzania, takribani wiki tatu zijazo majengo hayo 
yatazinduliwa rasmi baada ya kuwa yamekamilika”. Akasema Bw. Meroe
Baadhi
 ya changamoto hizo kwa upande wa iliyokuwa ICTR ni pamoja na 
kutokamatwa hadi sasa kwa watuhumiwa watatu ambao inaelezwa wapo 
mafichoni. Ni
 pili ni mahali pa kuwapeleka watu ambao ama wamekwisha maliza kutumikia
 vifungo vyao na kuachiwa huru. Watu hao wamekosa nchi ya kuwapokea na 
hadi sasa bado wanaendelea kuishi nchini Tanzania.
Na kwa
 sababu hiyo, Rais wa IRMCT ametoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kutoa 
ushirikiano wa kuwachukua watu hao ambao hawana mahali pa kwenda na kwa 
wale walioko mafichoni nchi ambazo wamejificha watoe ushirikiano kwa 
kuwafichua na kuwakamata ili hatimaye sheria iweze kuchukua mkondo wake
Kwa 
upande wake, Tanzania kupitia Mwakilishi wake katika Umoja wa Mataifa, 
Balozi Tuvako Manongi, amesema Tanzania inakaribisha kuhitimishwa kwa 
ujenzi kwa ujenzi wa makazo mapya ya iliyokuwa ICTR katika eneo la 
Lakilaki ndani ya wakati na kwa bajeti iliyopangwa.
“Kwa 
namna ya pekee tunampongeza Msajili wa Mahakama, Bw. John Hopkins kwa 
uongozi wake na ushirikiano wake ambao umewezesha kukamilisha hatua hii 
muhimu sana”. Akasisiza Balozi.
Aidha 
kukamilika kwa majengo hayo na ambayo yapo katika ardhi ya Tanzania ni 
heshima na fahari kubwa na ya kipekee kwa Tanzania na wananchi wake 
kutokana na jukumu kubwa iliyobeba ya kuwa mwenyeji wa Mahakama ya 
Kimataifa ya mauaji ya Kimbari ya Rwanda kwa niaba ya Jumuiya ya 
Kimataifa. 
Balozi
 Manongi pia amepongeza uratibu uliosimamiwa na Umoja wa Mataifa kupitia
 Ofisi ya Mshauri wa Sheria, Ofisi ya Msajili na the Hegue ya 
kuhakikisha kwamba, pamekuwapo na utaratibu mzuri wa kurithishana kutoka
 ICTR kwenda IRMCT. Na kwamba kazi hiyo haikuwa nyepesi.
Akizungumzia
 kuhusu kazi za IRMCT, Balozi amesema, Tanzania ingependa kuona Taasisi 
za Kitaifa zinawezeshwa ili ziweze kushughulikia kwa ukamilifu, haki na 
usawa na kwa kuzingatia sheria za kimataifa kesi zinazopelekwa kwenye 
Taasisi hizo za kitaifa.Aidha
 akasema uzoefu ambao umepatikana kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na 
ICTR pamoja na ile ya ICTY ni vema ukatumika kama mfano katika Mahakama 
nyingine za Kimataifa.
Kwa 
upande wa mashahidi, Tanzania imesisita umuhimu wa mashahidi kulindwa na
 kuhakikishiwa usalama wao dhidi ya vitisho mara baada ya kutoa 
ushahidi.Kuhusu
 watu walioachiwa huru baada ya kukamilisha vifungo vyao na bado wapo 
nchini Tanzania. Tanzania imeungana na wazungumzaji wengine katika 
mkutano huo wa kutaka pawepo na majadiliano ya kina ya kuangalia namna 
gani ya kuwasaidia watu hao.
Vile 
Tanzania imetoa wito kwa nchi zile ambazo zinahisiwa kwamba 
zinawahifadhi watuhumiwa watatu ambao wapo mafichoni na wanatakiwa 
kufikishwa katika vyombo vya sheria kutoa ushirikiano ili hatimaye haki 
itendeke.Watuhumiwa
 ambao wametajwa kuwa walihusika kwa namna moja ama nyingine katika 
mauaji ya Kimbari nchini Rwanda na wapo mafichoni hadi sasa ni Augustin 
Bizimana, Felicien Kabuga na Proitas Mpiranya. 
Kwa 
mujibu wa Ripoti iliyowasilishwa mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa 
Mataifa, watuhumiwa hao watakapopatikana kesi zao zitafanyika katika 
Mahakama hiyo mpya nchini Tanzania.Uamuzi
 kwa kuwa na matawi ya IRMCT huko Arusha na the Hague, Uholanzi 
unatokana na maamuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitia 
azimio nambari 1966 la mwaka 2010.
Kupitia
 Azimio hilo Baraza la Usalama liliamua kwamba, baada ya kumalizika 
rasmi kwa ICTR ( 2015) na ICTY ( 2017) Tanzania ambayo ndiyo ilikuwa 
mwenyeji wa ICTR itapewa jukumuu la kuhifadhi kumbukumbu na nyaraka zote
 muhimu za iliyokuwa ICTR ikiwa ni pamoja na kumalizia kesi zitakazokuwa
 zimebaki. Huku the Hague ikiwa na dhamana hiyo hiyo kwa kazi zilizokuwa
 za iliyokuwa ICTY.
Mahakama
 za Kimataifa za Rwanda na Yugoslavia ambazo zimefanya kazi kubwa ya 
kuwafikisha mbele ya sheria watuhumiwa karibu wote waliohusika na 
matukio ya kutisha ya ukiukwaji wa haki za binadamu ziliazishwa mwaka 
1990 na Umoja wa Mataifa
UMOJA WA MATAIFA WAISHUKURU SERIKALI YA TANZANIA
 
                    Reviewed by crispaseve
                    on 
                    
01:49
 
                    Rating: 
                    
Post a Comment