Header AD

RAMBO AHITIMISHA MAZISHI YA MWANAWE......



STAA, Sylvester Stallone Rambo, amemzika mtoto wake wa kwanza, Sage Stallone, ambaye alifariki baada ya kumeza madawa mengi.

Sage ambaye amewahi kuigiza na baba wake katika filamu ya Rocky V, alifariki dunia mapema mwezi huu ikiwa ni siku chache kabla ya kufunga ndoa.

Chanzo cha kifo chake hakijathibitishwa na daktari, isipokuwa maiti yake ilikutwa pembeni ya chupa tupu za vidonge zipatazo hamsini. Sage amefariki akiwa na umri wa miaka 36.

Kama alivyo baba yake, naye alikuwa mwigizaji, mwongozaji na mtayarishaji wa filamu.
Reviewed by crispaseve on 12:05 Rating: 5

No comments

Post AD