Header AD

BOMOA BOMOA YAANZA TENA MABONDENI DAR

 Moja ya nyumba za wakazi wa  eneo la Hananasifu, Kinondoni, ikiwa imebolewa katika operesheni ya kubomoa nyumba zilizopo katika bonde la Mto Msimbazi, Dar es Salaam. ambapo takriban ya nyumba 140 zilibomolewa na Kampuni ya Udalali ya Zumba, kwa tahadhari ya kuepukana na majanga ya mafuriko yatakayotokana na mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha kuanzia mwezi huu.
                            Mmoja wa wakazi wa eneo hilo akihamisha godoro

Wakazi wa eneo hilo wakiwa wamebeba kabati baada ya nyumba yao kukumbwa na bomoabomoa hiyo.
                                    Ilikuwa ni hekaheka kila mahala kunusuru vitu vyao
 Fundi wa kukodiwa wa Kampuni ya Udalali ya Zumba akibomoa ukuta wa nyumba moja katika eneo hilo.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kanda ya Kinondoni, Kamishna Msaidizi (ACP), Charles Kenyela, akiwa eneo la Hananasifu kusimamia ubomoaji wa nyumba hizo Dar es Salaam jana, ambapo takriban ya nyumba 140 zilibomolewa na Kampuni ya Udalali ya Zumba.
 Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), wakiimarisha ulinzi wakati wa uboaji huo.
 Mafundi wa kukodiwa wa Kampuni ya Udalali ya Zumba wakibomoa moja ya nyumba katika eneo hilo.
                                                      Baadhi ya vyombo vikiwa nje
                                                  Baadhi ya nyumba zilizobolewa
Mama akiwa amembeba mtoto wake huku akiangalia vyombo vyake baada ya nyumba aliyokuwa akiishi kubomolewa.
Reviewed by crispaseve on 10:17 Rating: 5

No comments

Post AD