USIRI WATAWALA JUU YA MZEE MANDELA
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amefutilia mbali ziara yake ya
kwenda Musumbiji baada ya kumtembelea hospitalini aliyekuwa Rais wa Afrika
Kusini, Nelson Mandela.
Rais Zuma amesema kuwa Bwana Mandela yuko katika hali
mbali ya afya.
Msemaji wa Zuma Mac Maharaj amesema kuwa hali yake imedorora zaidi katika saa
48 zilizopita.
Mandela ambaye, ni rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, amelazwa
hospitalini tangu tarehe 8 mwezi Juni akiugua maradhi ya mapafu.
Madaktari wanasemekana kufanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa Mandela
anapona.
Vikundi vya watu wenye huzuni mkubwa kuhusu hali ya afya ya Mandela,
walikusanyika nje ya hospitali alikolazwa, wakiwa na ujumbe wa ugua pole kwa
Mandela
Wadadisi wanasema kuwa wananchi wa Afrika Kusini wanaonekana kuwa tayari kwa
habari zozote sasa kuhusu hali ya Mandela.
"tutasikitika sana ikiwa tutapata habari za kifo chake, lakini pia tutakuwa
tunasherehekea maisha yake. Amefanya mambo mengi zaidi kwa nchi yetu,'' alisema
kijana John Ndlovu, mwenye umri wa miaka 25.
Zuma alitarajiwa kuhudhuria mkutano wa marais nchini Msumbiji, hii leo lakini
akaamua kuakhirisha safari yake.
Taarifa kutoka kwa ofisi yake ilisema kuwa anaendelea kuwapongeza wananchi wa
Afrika Kusini wanaoendelea kuiombea familia ya Madiba.
Uamuzi wa Rais Zuma kufutilia mbali ziara yake ambako alitarajiwa kuhudhuria
mkutano wa kikanda kuhusu uekezaji anaonyesha wazi kuwa hali ya Mandela
inaendelea kuzorota zaidi kulingana na mwandishi wa BBC mjini Johannesburg Mike
Wooldridge.
Reviewed by crispaseve
on
09:54
Rating:
Post a Comment