WANAFUNZI WALIOSOMA SHULE ZA KATA MPAKA VYUO VIKUU WATOA SHUKRANI ZAO KWA MH. LOWASSA
Waziri Mkuu mstaafu na Mbunge
wa Monduli, Edward Lowasa akisalimiana na wanafunzi wa chuo kikuu cha
UDOM waliotoka shule za sekondari za kata, wakati walipofika nyumbani
kwake mkoani Dodoma kutoa shukrani zao kwa hatua waliyofikia kielimu.
Na Father Kidevu Blog, Dodoma
Pia
wameahidi kujichangisha fedha kwa ajili ya malipo ya fomu hizo endapo
italazimika. Kauli hiyo ya kwanza kutoka kwa makundi na watu wasiokuwemo
ndani ya siasa, ilitolewa Jumatatu usiku nyumbani kwa Lowasa mjini
Dodoma, wakati kundi la wanafunzi hao walipofika kutoa shukrani zao kwa
hatua waliyofikia ikiwa ni matunda ya shule hizo, ambazo muasisi wake ni
mbunge huyo wa Monduli.
“Mimi
ninayofuraha kusimama hapa leo hii, nikiwa mtu tofauti, kwa maana
ninayesoma elimu ya juu, baada ya kufanikiwa ,kuendelea na elimu ya
sekondari kupitia shule za kata pale Kiluvya Dar es Salaam” anasema
Hamida Salum ambaye kwa sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza hapo UDOM.
Lowasa
wakati akiwa waziri mkuu wa Tanzania, kwenye mwanzoni mwa awamu ya n ne
ya utawala wa rais Jakaya Kikwete, aliweza kusimamia ujenzi wa shule za
kata kote nchini, ili kutoa nafasi zaidi za wanafunzi wa makabwela,
walioishindwa kendelea na masomo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja
na uhaba wa madarasa.
Kwa
sasa shule hizo zimekuwa zikibezwa na watu mbalimbali kwa maelezo kuwa
hazina walimu wa kutosha na uhaba wa vifaa vya kufundishia ikiwemo
vyumba vya maabara.
Kwa upande wake, Lowasa ambaye alikuwa pamoja na naibu waziri wa kazi na ajira, Dkt. Makongoro Mahanga, mbunge wa Kigoma mjini, Peter Serukamba, na mkuu wa mkoa wa Singida, Parseko Kone, aliwapongeza wanafunzi hao kwa moyo wao wa shukrani na kuwataka wasikatishwe tama na maneno yanayotolewa juu ya ubora wa shule hizo, kwani yeye binafsi anajivunia juhudi zake kupitia sera za chama cha Mapinduzi, zimeweza angalau kutoa wanafunzi wengi kutoka shule hizo kujiunga na vyuo vikuu.
Reviewed by crispaseve
on
16:02
Rating:
Post a Comment