Header AD

WAZIRI MKUU ATOA SH. MILIONI 10 KUSAIDIA VIJANA 87 WAJITEGEMEE

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameahidi kutoa sh. milioni 10 ili kuwasaidia vijana wanaoishi kwenye kijiji cha vijana cha Tulu ambao wameamua kujitegemea kwa uzalishaji kupitia kilimo, matumizi ya misitu na ufugaji.
Alitoa ahadi hiyo jana jioni (Alhamisi, Agosti 29, 2013) wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara na vijana wa kijiji hicho pamoja na wakazi wa vijiji jirani vya Tumbili na Lufwisi wilayani Sikonge mkoani Tabora.
Kijiji cha Vijana cha Tulu ambacho wenyewe wanakiita Pathfinders Green City (Jiji la Watafuta Njia) kilianzishwa Aprili 2013 kikiwa ni msitu mtupu baada ya kupewa ekari 280 kutoka vijiji jirani vya Tumbili na Lufwisi. Kilianzishwa kikiwa na vijana 68 kutoka katika kata zote 17 za Wilaya ya Sikonge. Hivi sasa kijiji kina vijana 87 wakiwamo wasichana 22 na wavulana 65 wenye umri wa kati ya miaka 18 na 24.
Reviewed by crispaseve on 09:34 Rating: 5

No comments

Post AD