Header AD

WANAFUNZI WA UDAKTARI MUHIMBILI HATARINI


-AMA KWELI MGANGA HAJIGANGI
WANAFUNZI wanaosomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (Muhas) wanaishi katika mazingira hatarishi kwani wanaweza kupata magonjwa ya mlipuko na yale ya kuambukizwa wakati wowote.

Uchunguzi uliofanywa na Operesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers ndani ya majengo ya chuo hicho yaliyo karibu na taasisi ya mifupa (MOI), umegundua kwamba kwa miezi mingi, vyoo vinavyotumiwa na wanafunzi hao vimejaa na kuziba kabisa, hali inayowafanya vijana hao, licha ya kushindwa kupata huduma hiyo muhimu ya kibinadamu, pia kuwa katika hatari ya kupatwa na magonjwa ya mlipuko.
“Hali ni mbaya sana hapa kwa kweli. Hatuna huduma ya choo kwa miezi miwili hadi mitatu sasa, tunapobanwa na haja, hasa kubwa, hulazimika kukimbilia Kariakoo kwenye vyoo vya kulipia, hapa hapafai,” mmoja wa wanachuo hao aliiambia OFM na kuomba hifadhi ya jina lake.
Wanafunzi hao ambao walitoa ushirikiano wa kutosha kwa makachero wetu, pia walisema majengo mengi yanayotumiwa kama mabweni yao ya kulala, yamechakaa na hivyo kuwafanya wawe na hofu kubwa, kwani yanaweza kuanguka wakati wowote.
WANAFUNZI WA UDAKTARI MUHIMBILI HATARINI WANAFUNZI WA UDAKTARI MUHIMBILI HATARINI Reviewed by crispaseve on 06:02 Rating: 5

No comments

Post AD