KINANA ATEMBELEA WANANCHI PEMBEZONI MWA WILAYA YA NKASI, AKUMBANA NA CHANGAMOTO ZA UBOVU WA BARABARA
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana
akiwafurahia vijana aliowakuta wakifanya kazi katika kijiji cha
Wampembe kilichopo kilometa 100 kutoka mji mdogo wa Namanyere wilayani
Nkasi. Vijana hao wanafanyakazi katika sekta ya afya na ujenzi.Pichani
kulia ni Mganga Mkuu wa Kituo hicho, Dk. Mwabulambo Gwamaka,Injinia wa
maji wilaya ya Nkasi,Bwa.Simon Sadala,Fundi Mkuu Ujenzi,Bwa.Athanael
Rwamlema na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Nkasi,Bwa.Kimulika
Galikunga.
Ndugu
Kinana
akikagua ujenzi wa Kituo Cha Afya cha Wampembe wilayani Nkasi mkoani
Rukwa akipata maalezo mafupi kuhusiana na ujenzi wa kituo hicho cha afya
kuyoka kwa Mganga Mkuu wa Kituo hicho, Dk. Mwabulambo Gwamaka.Kituo
hicho kimejengwa kwa msaada mkubwa wa Africare kwa kushirikiana na Plan
International,ambacho ni maalum kwa ajili ya afya mama na watoto na
upasuaji
Sehemu ya jengo la kituo cha Afya kikiendelea na ujenzi katika kijiji cha Mwampembe,wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa.
Wananchi wakishangilia jambo kwenye mkutano huo.
Pichani
Kinana akizungumza na wananchi katika kijiji cha Wampembe, jana,Aprili
Mosi, 2014. Na zinazoendelea ni picha zaidi za ziara hiyo na changamoto
hizo alizokumbana nazo kama zilizvyopigwa na Bashir Nkoromo aliyeko
kwenye ziara hiyo.
Katibu
Mkuu wa CCM ,Ndugu Abdulrahman Kinana jana, aliendelea na ziara yake katika
mkoa wa Rukwa, kwa kutembelea wananchi walioko pembezoni mwa mkoa huo,
ambapo alifika hadi katika Kata ya Wampembe iliyopo zaidi ya kilometa
100 kutoka mji mdogo wa Namanyere wilaya ya Nkasi iliyomo kata hiyo.
Katika safari iliyomchukua zaidi ya saa tisa, Kinana na msafara wake
alikumbana na changamoto kubwa ya ubovu wa barabara kutoka Namanyere
hadi kwenye vijiji vya kata hiyo kutona na magari kunasa mara kwa mara
kwenye tope na makorongo,kwa kuwa barabara haijapata kufanyiwa
matengenezo kwa muda mrefu.
Kufuatia kujionea changamoto hiyo, Kinana amewambia wananchi wa vijiji
vya Wampembe na Ntemba, kuwa ataishauri serikali kuifanya barabara hiyo
iwe chini ya Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) badala ya sasa ambapo
ipo chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi na hivyo kuwa vigumu
kupatikana fedha za kutosha kujenga barabara hiyo.
Kinana
akizungumza na wananchi saa mbili usiku, baada ya kuzuia msafara wake
eneo la kijiji cha Ntemba kaya ya Kate akitoka Kata ya Wampemba kwenda
Sumbawanga mjini.
KINANA ATEMBELEA WANANCHI PEMBEZONI MWA WILAYA YA NKASI, AKUMBANA NA CHANGAMOTO ZA UBOVU WA BARABARA
Reviewed by crispaseve
on
08:02
Rating:

Post a Comment