Header AD

KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA AWASILI WILAYA YA KALIUA,AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

 Katibu MKuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM,Wilaya ya Kaliua,katika ukumbi wa Millenium mkoani Tabora mara baada ya kupokea taarifa mbalimbali za maendeleo ya miradi na hali ya kisiasa wilayani Kaliua. Kinana yupo mkoani Tabora kwa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya CCM, kukagua maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
 Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Usindi  wakishuhudia Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikagua mradi wa ujenzi wa jengo la Zahanati ambayo tayari imwekwishakamilika,isipokuwa inasubiri kibali na kukamilika nyumba ya mganga.Kinana ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenenezi Nape Nnauye,ambapo walipokelewa na Mbunge wa jimbo la Urambo Magharibi,Mh.Prof Juma Kapuya 
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipata taarifa fupi juu ya mradi wa ujenzi wa jengo la nyumba ya Mganga wilayani Kaliua katika kijiji cha Usindi,Kata ya Ushokora,Katika ziara hiyo ya siku 11,Kinana ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenenezi Nape Nnauye,ambapo walipokelewa na Mbunge wa jimbo la Urambo Magharibi,Mh.Prof Juma Kapuya .
  Katibu Mkuu wa CCM,dugu Kinana  akilakiwa na Mbunge wa jimbo la Urambo Magharibi,Mh.Prof Juma Kapuya,mara baada ya kuwasili wilayani Kaliua,katika kijiji cha Usindi kata ya Ushokora akiwa ameambatana na  Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenenezi Nape Nnauye (hayupo pichani). mkoani Tabora.
Mbunge jimbo la Urambo Mashariki,Mh.Samwel Sitta akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Urambo Magharibi Prof.Juma Kapuya mapema leo kwenye wilaya ya Kaliua,mara baada uusindikiza msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana aliyekuwa Wilayani Urambo Mashariki kwa ziara ya siku 11 ndani ya mkoa wa Tabora.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipokelewa katika kijiji cha Usindi,Kata ya Ushokora wilayani Kaliua mkoani Tabora mapema leo asubuhi,akiwa ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenenezi Nape Nnauye na kupokelewa na Mbunge wa jimbo la Urambo Magharibi,Mh.Prof Juma Kapuya 
 Ndugu Kinana pichani na viongozi wengine wa CCM,wakienda kukagua Mradi wa ujenzi wa Zahanati na nyumba ya Mganga,katika kijiji cha Usindi kata ya Ushokora wilayani Kaliua mkoani Tabora.
  Ndugu Kinana  wat tatu kulia akizungumza jambo na  Mbunge wa jimbo la Urambo Magharibi,Mh.Prof Juma Kapuya,kulia ni   Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenenezi Nape Nnauye  na viongozi wengine wa CCM,wakitoka kukagua Mradi wa ujenzi wa Zahanati na nyumba ya Mganga,katika kijiji cha Usindi kata ya Usindi wilayani Kaliua mkoani Tabora.
KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA AWASILI WILAYA YA KALIUA,AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA AWASILI WILAYA YA KALIUA,AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO Reviewed by crispaseve on 07:37 Rating: 5

No comments

Post AD