Header AD

MAN CITY YANUSA UBINGWA WA EPL, YAIGONGA BAO 4 – 0 ASTON VILLA

Man CityManchester City imeonyesha nia ya dhati kabisa ya kutaka kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya England ‘EPL’ baada ya kuipa kipigo cha mabao 4 kwa nunge klabu ya Aston Villa katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Etihad hapo jana
Mabao mawili ya mwanzo ya City yalifungwa na  Dzeko, Stevan Jovetic aliyefunga goli la tatu kabla ya kiungo tegemezi wa timu hiyo ‘Yaya Toure’ kupachika bao la nne mnamo dakika ya 90 na kuiwezesha timu yake  kuibuka kidedea kwa ushindi huo mnono.
City
 Wachezaji  wa City wakishangilia baada ya kipenga cha mwisho kupulizwa.
Ushindi  walioupata City umewaweka kilele mwa ligi hiyo  kwa tofauti ya pointi mbili dhidi ya Liverpool ambayo kwa sasa inakamata nafasi ya pili ikiwa na pointi 81 huku ikiwa imebakisha mchezo mmoja mkononi.
Kwa upande wa Liverpool yenyewe  bado inakibarua kigumu  hasa baada ya  matokeo ya ushindi waliyoyapata City dhidi ya Aston Villa. Majogoo hao wa jiji la London watavaana na Newcastle jumapili ijayo.
Steven JoveticSteven Jovetic wa Manchester City akishangilia bao alilofunga
PelleghiriniMashabiki wa City wakiwa na bango kubwa lenye picha ya kocha wa klabu hiyo Manuel  Pellegrini.
Tazama Video za magoli hapo chini
MAN CITY YANUSA UBINGWA WA EPL, YAIGONGA BAO 4 – 0 ASTON VILLA MAN CITY YANUSA UBINGWA WA EPL, YAIGONGA BAO 4 – 0 ASTON VILLA Reviewed by crispaseve on 06:46 Rating: 5

No comments

Post AD